Wanafunzi DSJ walia na tamasha la vipaji - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Thursday, 30 March 2017

Wanafunzi DSJ walia na tamasha la vipaji



                                                     
Husna Hassani,Dar es Salaam

WANAFUNZI wa chuo cha uandishi wa habari Dar es Salaam (DSJ) wameutaka uongozi wa serikali ya wanafunzi kuandaa mashindano mengi zaidi ili kuweza kuibua vipaji .

Akizungumza na mwandishi wa habari hii Jabir Hamis ambaye ni mwanafunzi wa ngazi ya cheti alisema kuwa kuna umuhimu wa kuwa na mashindano mengi zaidi ambayo yanaleta hamasa kwa wengi kuonesha vipaji vyao.

“Ushindani ni kitu kizuri kwani unaibua ujuzi wa kila mwanafunzi kuweza kupata muda wa kuonyesha kile alicho nacho pamoja na kutoa fursa kwa wanafunzi kuweza kutambua uwezo wao kimasomo katika kuonesha kile wanachopenda kufanya “alisema
Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Dar es Salaam wakijipatia chakula katika siku ya tamasha la wanafunzi (Bash) viwanja vya Jangwani See Breeze Dar es Salaam
 .
Shamimu Abel  alisema kuwa kuna kila sababu za uongozi kujali vipaji vya wanafunzi kwa kuwaendeleza zaidi katika yale wanayojifunza na kuhakikisha kuwa kila mmoja anaishi kwenye malengo aliyojiwekea.

Ally Makame ambaye ni naibu waziri wa michezo alisema kuwa mpango mzima wa kutambua vipaji na matamasha ni mwendelezo ambao utasimamiwa na serikali ya wanafunzi kwa kushirikiana na uongozi wa chuo kuhakisha kuwa vipaji vinaibuliwa zaidi.

“Tunatambua umuhimu wa vipaji kwa wanafunzi na maandalizi zaidi yanafanyika ili kuhakikisha kuwa tunaweza kujua uwezo waliona hiyo ni kazi tunayoifanya kwa kuwajali wanafunzi wote katika suala zima la taaluma”alisema

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad