Na.Jabiri Hamisi,Dar es Salaam
TIMU ya mpira wa miguu ya chuo cha uandishi wa habari Dar Es
Salaam (DSJ) inajipanga kulipa kisasi kilicho dumu kwa mwaka mmoja dhidi ya
timu ya wanahabari kutoka Azam katika mechi ya Kirafiki itakayopigwa viwanja
vya Mabibo.
| Kiungo wa timu ya DSJ star (Kulia) Gery Gerad akionesha uwezo kwenye mchezo wa kirafiki kati ya Azm media na DSJ Star |
“Wanahabari wenzentu Azam hivyo sisi ni familia moja waliacha
kilio kwetu kwa kutufunga magoli matano tunawakumbuka na uwezo wao
tunautambua wajipange tu kuhakikisha wanabeba mzigo wa kutosha wa magoli
“alisema Makame
Vaileth Mawaka mwakilishi kutoka Azam alisema kuwa lengo
kubwa la michezo ni kuimarisha ushirikiano na kuhakikisha kuwa kila mmoja
anapata nafasi ya kuwa mwanafamilia
na kuimarisha mahusiano baina ya wanamichezo.
“Hakuna anayependa kushindwa ila kwetu mchezo ni zaidi
ya urafiki kwani inatufanya tuboreshe mahusiano zaidi na kufungua uwanda mpana
pamoja na kupata nafasi ya kupumzisha akili kwani muda mwingi tumekuwa
tukifanya kazi ya kuhabarisha jamii”alisema Vaileth.
No comments:
Post a Comment