Ubinafsi unaua tasnia ya filamu - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Friday, 2 September 2016

Ubinafsi unaua tasnia ya filamu




KATIBU wa chama cha waigizaji Tanzania mkoani Pwani (TFDAA) Kadnas Nassoro amesema kuwa ubinafsi ni tatizo kubwa linalosababisha tasnia isiweze kufanya vema zaidi kwa wasanii wengi wa filamu na muziki nchini.
 Akizungumza  hivi karibuni amesema kuwa hali ya kila msanii kujiona yeye ni bora kuliko mwenzake na kutopenda kushirikiana na wasanii wengine kunawaponza wengi na kuwafanya washindwe kufanikiwa.
Katibu wa chama cha wasanii mkoani Pwani (TFDAA) Kadnas Nassoro


 “Kila msanii anataka kuonekana yeye ni bora kuliko wenzake katika tasnia hicho kitu hakitakiwi tunapaswa kushirikiana katika kila namna ili tuweze kudumisha umoja utakaotuletea mafanikio zaidi”alisema
 Naye Mwenyekiti wa TFDAA mkoa wa Pwani Vendavenda Sumuni amewataka wasanii wajitokeze kwa wingi kujiunga katika umoja huo ili wawe na sauti moja katika kufuatilia haki zao na kuhakikisha kila msanii
anafikia malengo.
 “Mkiwa na umoja ni sawa na kuwa na sauti moja yenye nguvu hali itakayofanya tuweze kufanya vizuri katika tasnia yetu na kuweza kusaidia kuinua vipaji zaidi hivyo nawasihi tuungane katika umoja huu”amesema

Pia Marrystell Abubakari aliongeza kwa kusema kuwa ili kazi ya sanaa iweze kukua inahitaji ubunifu wa hali ya juu na kutokata tamaa mapema kwa kuwa mafanikio sio kitu chepesi kama wengi wanavyofikiria.
Chama hicho kilianzisha mwaka 2011 chini ya Mike Sangu kikiwa na lengo la kuimarisha umoja wa wasanii kinasimamiwa na diwani wa kata ya Mtambani Mkoani Pwani wilaya ya Kibaha Godfrey Mwafulilwa .
Kina jumla ya wanachama 100 na kimeweza kusimamia uzalishaji wa filamu pamoja na tamthilia ya siri ya nafsi pamoja na filamu zilizopo sokoni ambazo ni pamoja na Bingo,Mzimu wa Nyangiti,who is he,heri ya jana na nyingine nyingi zinazofanya vizuri sokoni.

1 comment:

Post Top Ad