Na Mainda Mhando,Dar es Salaam
MKURUGENZI mtendaji wa Mtaasisi Media Group (MMG) Ambele
Mwafulango amewataka wanafunzi kutokukata tamaa katika suala zima la kujifunza
na kuhakikisha kuwa wanatumia muda vizuri.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii alisema kuwa siri
kubwa ya mafanikio ipo katika kuutawala muda vizuri na kuweka mpangilio wa
mambo kwa wakati.
Aliongeza kwa kusema kuwa katika kila jambo la mwanadamu
analofanya anategemea kujipanga na kuweka mipango kwa wakati hasa katika suala
zima la muda kwa kuwa umakini katika muda unaleta umakini katika utendaji.
Salama Ngale ambaye ni mlezi wa kundi hilo amesema kuwa
jambo kubwa la kufanya katika maandalizi ya muda na kuthamini kila jambo ili
kuhakikisha kuwa kila jambo linakwenda kwa mpangilio mzuri ili kuhakikisha kila jambo linakwenda kwa utaratibu.

No comments:
Post a Comment