N a Japhary Lesso,Dar es Salaam
Naibu waziri wa wizara ya Michezo wa serikali ya wanafunzi
kwa chuo cha uandishi wa habari Dar es Salaam (DSJ) amewataka wanafunzi
kutohofia kushiriki kwenye michezo na
mashindano yanayoandaliwa na chuo kwa kuwa ni fursa nzuri kutambua uwezo na
vipaji vyao.
Kikosi cha mpira wa miguu DSJ Stars |
Akizungumza na mwandishi wa habari hii chuoni hapo alisema
kuwa mashindano na michezo inayoandaliwa katika chuo cha uandishi wa habari
yana lengo la kuboresha na kuinua vipaji vya
wanafunzi chuoni hapo hivyo kila mmoja anapaswa kuwajitoa.
wanafunzi chuoni hapo hivyo kila mmoja anapaswa kuwajitoa.
“Hakuna haja ya kuhofia kuja na aina nyingine ya michezo
kwani kila mwanafunzi ana uhuru wa kuchagua na kuandaa michezo anayoipenda
tunatoa ushirikiano wa kutosha ili kuhakikisha kuwa hatuwekezi nguvu nyingi
kwenye mchezo wa mpira wa miguu pekee”alisema
Yahaya Jabiri mwanafunzi wa ngazi ya cheti alisema kuwa
serikali ya wanafunzi imewekeza nguvu nyingi kwenye mchezo wa mpira wa miguu
hali inayofanya kuacha aina nyingine ya michezo kudorora hivyo kuna haja ya
kuwekeza kwenye michezo ya aina nyingine pia.
“Wanathamini mchezo wa mpira wa miguu pekee na kushindwa
kutoa nafasi kwenye michezo mingine kama vile basketball,riadha pamoja na
michezo ya kuvutana kamba hali inayotufanya tushindwe kujifunza michezo mingine
kwani inatukosesha fursa ya ajira”alisema
No comments:
Post a Comment