TUSISAHAU KUWEKEZA NGUVU KUBWA KWA VIJANA - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Monday, 29 January 2024

TUSISAHAU KUWEKEZA NGUVU KUBWA KWA VIJANA


NGUVU kubwa kwenye soka la Tanzania inahitajika katika kila idara kutokana na maendeleo kuzidi kuonekana kila iitwapo leo. Hili ni kubwa na linapaswa pongezi kwa kuwa kila timu inaonyesha nia ya kufanya kweli.

Ambacho kinapaswa kuwa endelevu ni kwenye uwekezaji kwenye kila idara hili litaongeza nguvu ya ushindani. Ushindani ukiongezeka hata thamani ya soka pia inazidi kupanda kila wakati.

Sio kwa timu za wakubwa tu hapana ni muhimu hata kwenye timu za vijana nako pia nguvu ikawa kubwa hii itaongeza ushindani na upande wa ligi ya vijana ambayo ni mzizi wa kuwa na wachezaji wazuri wakati ujao.

Ukweli ni kwamba ngazi ya vijana ni muhimu kutazamwa kwa ukaribu ili kuongeza nguvu kwa kuwa hawa wanatengenezwa kwa ajili ya kutumika kesho kitaifa na kimataifa.

Kukiwa na ongezeko la wachezaji kutoka timu za vijana wakiwa wanapewa nafasi pia kwenye timu za wakubwa taratibu watazidi kuwa imara kwa ajili ya mashindano makubwa.

Ili kuwa na wachezaji wengi wazawa ambao watafanya vizuri katika timu ya taifa ya Tanzania ni muhimu kuwa na sehemu nyingi za kuwatengeneza hasa kwenye timu za ndani.

Ikiwa ni timu chache zitakuwa zinawekeza nguvu kwenye kuwatengeneza wachezaji vijana hili litakuwa ni gumu kuwa na wazawa wenye uwezo mkubwa wakati ujao.

Kufanya vizuri kwa timu ya taifa ya Tanzania kunahitaji uwepo wa mwendelezo wa vijana ambao wanaandaliwa kwa wakati huu katika mashindano mbalimbali.

Furaha ya vijana kufanya vizuri kwenye mechi na mashindano ambayo watakuwa wanashiriki italeta furaha kesho kwenye mashindano ya timu ya taifa ya Tanzania.

Ni muda wa kuongeza nguvu pia kwenye uwekezaji katika soka la vijana kwenye kila timu hii itafanya wachezaji wengi wazalishwe kuanzia ngazi ya chini.

Uwekezaji ukiwa mkubwa unatoa fursa kwa timu kubwa kuwapa nafasi wale wachezaji kutoka ngazi ya vijana kucheza mechi za kimashindano jambo litakalowaongezea hali ya kujiamini.

Vijana wana uwezo wa kufundishika na kuendelea kuwa kwenye mwendo bora katika mechi za kitaifa na kimataifa hili lipo wazi.

 Wale ambao watapewa nafasi pia ni muhimu kujituma kila wakati kuonyesha thamani ya kuaminiwa na benchi la ufundi katika mechi watakazopewa.

Kila timu ni wakati wake kuendelea kupambana kutengeneza wachezaji kwenye idara ya vijana nguvu ikiwa kubwa huku italeta matokeo mazuri.

Ikiwa hivyo hata kwenye mechi za kimataifa vijana wakiwa wanapewa nafasi watazidi kutambua namna hali ilivyo kwa kuwa ili uwe bora ni lazima ukutane na wapinzani bora kwa nyakati tofauti.

Kila kitu kinawezekana na muda bado upo kufanya maandalizi kwa ajili ya kesho bora kwa vijana waliopo nje na ndani ya timu.

Ukweli ni kwama mchezo wa mpira ni mchezo wa wazi hauhitaji mambo mengi zaidi ya uwekezaji na kufanya kweli kwenye mechi za kitaifa na kimataifa.

Vijana wakipewa nafasi wanaweza na wakiandaliwa kwa wakati huu itakuwa ni faida kubwa kwa kukua soka la Tanzania ambalo kila leo ushindani wake unazidi kuongezeka.

 

 

 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad