Ziara ya masomo DSJ yanukia Tanga - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Tuesday, 14 March 2017

Ziara ya masomo DSJ yanukia Tanga



                                                  
 Na.Agnes Mathew,Dar es Salaam

WAZIRI wa elimu kwa serikali ya wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Dar es Salaam(DASJOSO) Saitoti Mwalimu amewataka wanafunzi kushiriki ziara ya kimasomo itakayofanyika mkoani Tanga yenye lengo la kuongeza ujuzi kwa vitendo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii alisema kuwa kuna faida kubwa kwa wanafunzi kushiriki kikamilifu ziara ya kimasomo itakayofanyika mwezi wa nne kwa kuwa watapapata muda mzuri wa kubadili madhari na kuwa ni watalii wa ndani kwa kutembelea vivutio vya mkoani Tanga.

Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Dar es Salaam(DSJ) 
“Tunatembelea mkoa wa kitalii na wenye upekee itakuwa ni fursa kwa wanafunzi kujifunza kwa vitendo na kuweza kutembelea sehemu mbalimbali ambazo ni za kihistoria pamoja na kutembelea vyombo vya habari
vilivyo mkoani humo kwa muda wa siku nne”alisema.

Aidha alisema kuwa wanashirikiana na uongozi wa chuo ili kuhakikisha kuwa lengo la ziara linabaki kuwa la lenye misingi madhubuti na kusimamia ukweli na uwazi hasa katika matumizi ya fedha na yeyote atakayekiuka taratibu hatua za kinidhamu zitachukua mkondo wake.

Michel Fredy mwanafunzi wa ngazi ya cheti alisema kuwa kuna umuhimu kwa wanafunzi kuzingatia taratibu za chuo na kufuata sheria pasipo kupindisha mambo kwani tabia za kupuuzia huwaponza wengi hali inayopoteza ubora wa ziara.

1 comment:

Post Top Ad