PANGA KUPITA NA 11 NDANI YA KMC - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Wednesday, 5 July 2023

PANGA KUPITA NA 11 NDANI YA KMC


NDANI ya KMC yenye maskani yake Kinondoni panga kubwa linatarajiwa kupita kwa mastaa wao ili kuunda kikosi kipya cha ushindani.

Timu hiyo imebaki ndani ya Ligi Kuu Bara kwa ushindi kwenye mchezo wa mtoano KMC imewaandikia mastaa 11 barua za kuwapa mkono wa asante.


KMC ilibaki ndani ya ligi kwa ushindi wa jumla ya mabao 3-2 Mbeya City ambayo hii itashiriki Championship.

Mbeya City kwenye mchezo wa kwanza Uwanja wa Sokoine ilipata ushindi wa mabao 2-1 na mchezo wa pili wa kumsaka mshindi ikashuhudia ubao wa Uwanja wa Uhuru ukisoma KMC 2-0 Mbeya City.

Hivyo ni rasmi kuwa KMC bado wapo ndani ya ligi na wanatarajia kufanya maboresho makubwa kwenye kikosi hicho.

Ni wachezaji 11 wanatarajiwa kupewa mkono wa asante kwa ajili ya kuwapa nafasi nyota wengine wapya kwenye kikosi hicho.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad