AZAM Sports Federation Cup 2023/24 raundi ya pili inatarajiwa kupigwa ndani ya Januari baada ya ratiba kupangwa.
Kagera Sugar inayotumia Uwanja wa Kaitaba kwa mechi za nyumbani itamenyana na Dar City Januari 31 saa 10:00 jioni.
Mabingwa watetezi Yanga watavaana na Hausing FC Januari 30 Saa 1:00 usiku, Uwanja wa Azam Complex.
Mtibwa Sugar watamenyana na Nyakagwe FC, Januari 30 Uwanja wa Manungu Complex Saa 10:00 jioni.
Simba itacheza na Tembo FC Januari 31 ambapo muda na uwanja vitatajwa hivi karibuni.
No comments:
Post a Comment