TATIZO LA UMALIZIAJI LATAFUTIWA DAWA SIMBA - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Sunday, 10 April 2022

TATIZO LA UMALIZIAJI LATAFUTIWA DAWA SIMBA



SELEMAN Matola, Kocha Msaidizi wa Simba amesema kuwa kwa sasa wanafanyia kazi makossa ya wachezaji wao ikiwa ni pamoja na tatizo la umaliziaji wa nafasi ambazo wanazipata.

Mabingwa hao watetezi kwenye msimamo wapo nafasi ya pili wakiwa wameachwa pointi 11 na Yanga iliyo nafasi ya kwanza na pointi 51.

Matola amesema kuwa wanatambua kwamba kuna makosa ambayo yapo jambo ambalo wanalifanyia kazi kila wakati.

“Makosa yapo kwenye mechi ambazo tunacheza tunaona kwamba hata mchezo wetu dhidi ya Coastal Union tuliweza kupoteza nafasi ambaz tulizitengeneza hivyo hilo tunalifanyia kazi kwenye uwanja wa mazoezi,” alisema.

Wakati Simba ikishinda mabao 2-1 dhidi ya Coastal Union wachezaji wa timu hiyo walikosa nafasi 10 za kufunga ambazo ziliokolewa na kipa wa Coastal Union, Mussa Mbissa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad