Mkaa Mkombozi utaikomboa Tanzania kutoka kwenye jangwa - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Monday, 10 October 2016

Mkaa Mkombozi utaikomboa Tanzania kutoka kwenye jangwa




MABADILIKO ya hali ya hewa yamekuwa yakichangiwa kwa kiasi kikubwa na shughuli za binadamu wenyewe kama vile kilimo,ujenzi wa aina yopyote pamoja na ufugaji ambao huitaji maeneo makubwa ili kuwekeza hali inayopelekea kukata miti katika eneo husika.
     Katika awamu ya nne iliyokuwa  chini ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete ilikuwa ikitumia sera ya kata mti panda mti lengo kubwa ilikuwa ni kuitoa Tanzania katika hatari ya kuingia katika jangwa kubwa la ukame na kuweza kuyatunza mazingira.
Msimamizi wa CBTL Neema Kalenga akitoa ufafanuzi wa mkaa Mkombozi
      Kampeni ilipokewa vizuri kwani Taifa zima lilihamasika na kuanza kupanda miti katika maeneo mbalimbali waliyokuwa wakiishi na wale waliokuwa wakikata miti ili kuchoma mkaa nao pia kwa kiasi kikubwa walihusika kutunza mazingira kwa kupanda miti.
    Wimbo wa kila siku kwa nchi yetu ni kuanza vizuri kabisa katika mpango na kuishia kati kati bila kujua tulikoanza na tunakoelekea
hali inayofanya tuanze kurejea kulekule tulikotoka muda sio mrefu tena tukajisahau tukaendelea na shughuli zetu sera ikatupwa kule.
      Bado tatizo limekuwa kubwa ukataji wa miti umekuwa ukiongezeka tena kwa kasi zaidi kadri siku zinavyokwenda na matumizi ya mkaa yanazidi kupamba moto kwani jiji pekee la Dar es Salaam lenye wakazi wengi ndio kinara kwa kutumia mkaa cha kufurahisha ni kwamba hakuna msitu maalumu katika jiji.
       Kwa maana hiyo mkaa unaotumika katika jiji la Dar es Salaam unatoka mikoa ya karibu kama vile Morogoro,Iringa na Tanga huku ndiko misitu inavunwa na kutengeneza nishati ya mkaa kwa matumizi ya nyumbani.
      Baada ya kuligundua hilo kuwa ni tatizo katika bara la Afrika kiujumla kampuni ya  Charcoal Briquettes Tanzania limited (CBTL) wamekuja na mbinu mbadala kabisa ya kuokoa mazingira kwa kuyatunza na ukataji holela wa miti kwa kuzalisha mkaa unaoitwa Mkombozi.
Msimamizi na mtoa mafunzo wa mradi huo Neema Kalenga anaeleza namna walivyojipanga kuhakikisha kuwa wanaitunza ardhi ya Tanzania kwa kuiweka katika hali ya usalama zaidi kwa kutumia mbinu mbadala na rafiki wa mazingira
      Ili kuokoa mazingira yetu tumeanza kutengeneza mkaa ambao hautumii miti katika kuutengeneza hali inayofanya tuokoe miti mingi zaidi na kutengeneza mkaa bora kabisa kwa kutumia masalia ya taka za shamba katika kutengeneza mkaa alisema Neema
       Tunatengeneza mkaa kwa kutumia mabaki ya shambani kama vile mabua,nyasi za mpunga,vijiti vidogo vidogo pamoja na maranda ya mbao  tunazalisha mkaa safi kabisa na unafaa kwa matumizi ya nyumbani na kiwandani pia
      Lengo letu kubwa ni kuweza kuyatunza mazingira yetu kwa kuanza na mradi huu na tunatoa elimu kwa wananchi ili waweze kuutambua mkaa huu na kuutumia kwani haiuna madhara yoyote yale na ni kwa bei nafuu sana unajipatia mkaa huu aliongeza Neema
    Kuhusu mafunzo ya kutengeneza mkaa huo anaeleza kuwa walipata mafunzochini ya mkurugenzi Nachiket Potnis kutoka  India na walianza kufundisha mikoa kama vile Pwani kisha wakasogea Dar es Saalaam.Tanga na Morogoro lengo likiwa ni moja tu kutunza mazingira .
     Bado watanzania hawajaanza kuuelew mkaa kwani kuna mkaa mwingi sana katika stoo yetu hali inayotupa wasiwasi kuwa bado mazingira yanazidi kuharibika na miti inazidi kukatwa nawaomba watanzani waweze kubadilika na kuanza kutumia nishati rafiki wa mazingira alisisitiza Neema
Tunawafikia watanzania kwa kutumia mawakala wetu waliopo sehemu mbali mbali na pia kwa njia ya matangazo ili waweze kujua uwepo wetu sisi na kutumia bidhaa zetu wengi huhisi mkaa huu ni sawa na jiwe hivyo hauwezi kuwaka wao wanaogopa.
     Anafafanua namna unavyotengenezwa kwa kusema mabaki ya mimea hutengenezwa kuwa vumbi la mkaa kwa kutumia mitambo maalumu ya kutengenezea mkaa  kisha tunasindika mkaa na kuupooza katika vichanja kwa muda wa siku mbili au tatu tayari kwa matumizi
Wakulima ,wajasiriamali na vijana huwauzia mabaki hayo ya mimea katika maeneo waliyopo na kuwafanya waweze kuzalisha bidhaa kwa wingi katika viwanda vyao vilivyopo Bagamoyo na Mlandizi Mkoani Pwani.
     Anatoa wito kwa serikali na jamii kuweza kuwaunga mkono katika juhudi za kutunza mazingira ili kuwa na mazingira bora yatakayovutia  na kufanya tusiweze kuathirika kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya hali ya hewa kwani Tanzania ni yetu sote alisisitiza Neema alipokuwa akiongea na gazeti hili.
       Naye Diwani wa Kibaha kata ya Mail Moja Ramadhan Lutambi amewasihi wafanyabiashara kutengeneza bidhaa zenye ubora na kuziuza kwa bei nzuri ili wasimuumize sana mteja kwani katika mapambano haya kila mmoja lazima ahusike ipasavyo.
   
Jukumu la kutunza mazingira yetu ni la kila mmoja hivyo yatupasa kuwa wazalendo na nchi yetu tutunze mazingira yetu kwa kuwa ndi fahari ya taifa kuwa na mazingira bora kwa maendeleo ya watu wake alisitiza

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad