KIUNGO wa matajiri wa Dar, Azam FC Feisal Salum amekuwa kwenye ubora wake katika mechi za hivi karibuni ndani ya Ligi Kuu Bara akifanya kazi kubwa kwenye kutimiza majukumu yake.
Yote haya
yanatokana na ushindani uliopo uwanjani huku Fei Toto akikamilisha kazi yake
kwa umakini na kuwapa furaha mashabiki wa Azam FC wanaoifuatilia timu hiyo
inayotumia Uwanja wa Azam Complex kwenye mechi za ushindani.
Nyota huyo
anayevaa jezi namba 6 mgongoni ni chaguo la kwanza la Kocha Mkuu, Yusuph Dabo raia
wa Senegel ambaye ameweka wazi kuwa kila mchezaji ndani ya kikosi hicho ana
nafasi ya kufanya vizuri na makosa ambayo yamekuwa yanatokeo uwanjani
wanayafanyia kazi eneo la mazoezi.
Azam FC
imekuwa na mwendo mzuri kwenye mzunguko wa pili kwa kupata pointi kwenye mechi
zote walizocheza Uwanja wa Azam Complex na safu ya ushambuliaji ikifunga mabao
matano kwenye mechi mbili walizocheza wakiwa nyumbani.
Dabo
amesema: “Kazi kubwa inafanyika kwa kila mchezaji kutimiza majukumu yake na ipo
hivyo kila wakati jambo ambalo linaongeza nguvu kwenye kutimiza majukumu yetu
na kupata ushindi ndani ya uwanja.
“Wakati
mwingine tumekuwa tukishinwa kupata matokeo jambo ambalo linatokea hivyo
kikubwa ni kuona tunakuwa kwenye mwendelezo mzuri kwa kuwa kinachohitajika ni ushindi
na tunatambua kwamba ushindani ni mkubwa.
“Sio Feisal
pekee bali kila mchezaji anatimiza majukumu yake hili ni jambo la msingi, pale
ambapo tunashindwa kupata matokeo makosa tunafanyia kazi eneo la mazoezi ili
kuwa bora kwa mechi zinazofuata,”.
Fei Toto
kwenye mechi mbili zilizochezwa Uwanja wa Azam Complex alifunga jumla ya mabao
matatu. Ubora wa Fei Toto ulichangia kupatikana kwa pointi nne kati ya pointi
sita ambazo zilikuwa zinasakwa uwanjani ndani ya dakika 90.
Nyota huyo
alifunga mabao mawili kwenye mchezo dhidi ya Dodoma Jiji uliochezwa Uwanja wa
Azam Complex ambao baada ya dakika 90 ubao ulisoma Azam FC 4-1 Azam FC
walipokomba pointi tatu jumlajumla.
Mchezo wa
pili kufunga bao ilikuwa dhidi ya Coastal Union uliochezwa hapohapo Azam
Complex ilikuwa ni Machi 6 ubao wa uliposoma Azam FC 1-1 Coastal Union wababe
hao wakagawana pointi mojamoja.
Kwenye
mchezo dhidi ya Coastal Union alifunga bao lililowapa pointi moja dakika za
jioni kwa kuwa Azam FC walikuwa nyuma kwenye mchezo huo uliokuwa na ushindani
mkubwa dhidi ya Wagosi wa Kaya kutoka Tanga.
Fei alifunga
bao hilo dakika ya 81 akiweka usawa bao ambalo lilifungwa na Semfuko Charlse
dakika ya 68. Jumla anafikisha mabao 12 kwenye ligi akiwa ni kinara wa utupiaji
mabao.
Mechi 20
Azam imecheza kwenye ligi ikiwa nafasi ya kwanza kibindoni imekusanya pointi 44
na safu ya ushambuliaji imetupia jumla ya mabao 45 msimu wa 2023/24.
Ikumbukwe
kwamba licha ya kuwa ni kinara wa mabao akiwa nayo 12 kwenye ligi Fei ni mfungaji
wa bao la kwanza ndani ya Azam FC kwenye ligi ilikuwa dhidi ya Tabora United
mchezo uliochezwa Uwanja wa Azam Complex.
Katika
mchezo huo bao la Fei Toto la ufunguzi lilifungwa dakika ya 3 ikiwa ni mwanzo
wa msimu wa 2023/24 na rekodi nyingine aliyonayo ni mfungaji wa kwanza hat
trick ndani ya Ligi Kuu Bara msimu wa 2023/24 alipofunga kwenye mchezo dhidi ya
Tabora United.
Kazi kubwa
ni kwenye mwendelezo wa kusaka pointi tatu ndani ya ligi huku kiungo huyo
akiweka wazi kwamba kila mchezo kwao wanauchukulia kwa umuhimu ili kupata ushindi.
“Kila mchezo
tunashirikiana na wachezaji wote ili kupata pointi tatu muhimu pale ambapo
tunakosa huwa tunarejea kwenye uwanja wa mazoezi kufanyia kazi makosa yetu hiyo
huwa inakuwa kazi ya benchi la ufundi kwenye kufanya maboresho yetu.
“Ushindani
ni mkubwa na bado tunaendelea kushindana ili kupata matokeo, mashabiki wazidi
kuwa pamoja nasi kwa kuwa kila wakati wapo nasi bega kwa bega katika hilo
tunawaomba waendelee kuwa nasi,”
No comments:
Post a Comment