SIMBA na Yanga zimetinga hatua ya robo fainali Ligi ya Mabingwa Afrika rekodi kubwa na ya kujivunia kwa Tanzania kwenye ulimwengu wa mpira.
Kufika kwao hatua ya nusu fainali ni mipango makini na maandalizi mazuri mmoja kati yao huenda atakutana na Mamelod Sundowns hawa miamba kabisa kutoka Afrika Kusini.
Droo inatarajiwa kuchezwa hivi karibu ambapo Simba haitakutana na ASEC Mimosas kwa kuwa walikuwa kundi moja kama ilivyo Yanga haitakutana na AL Ahly ya Misri.
Kila mmoja kwa nyakati zake ametimiza majukumu yake ambapo Pacome anaingia kwenye rekodi ya kuwa mchezaji pekee aliyefunga bao dhidi ya Al Ahly kwenye hatua ya makundi mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika uliochezwa Uwanja wa Mkapa.
Chama kwenye mchezo dhidi ya Jwaneng Galaxy alikuwa na siku nzuri kazini alipofunga bao moja na kutoa pasi moja ya mchezo wakati Simba ikifanikisha malengo ya kutinga hatua ya robo fainali Ligi ya Mabingwa Afrika.
No comments:
Post a Comment