Yatima wamliza Joyce Mbogo - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Monday, 17 October 2016

Yatima wamliza Joyce Mbogo




MRATIBU wa masomo wa chuo cha uandishi Dar es Salaam (DSJ) Joyce Mbogo amesema kuwa jamii inapaswa kufanya tendo la kujitoa kuwa endelevu  na  kuwasaidia watoto yatima kwa kuwa uhitaji wao ni mkubwa na wanahitaji faraja kutoka kwa watu wanaoizunguka jamii .
Mratibu wa masomo DSJ Joyce Mbogo (aliyeshika kichwa) akiwa na Mlezi wa Yatima



       Akizungumza na waandishi wa habari akiwa katika kituo cha watoto yatima cha Msimbazi Center kilichopo ilala jijini Dar es Salaam amesema kuwa kujitoa ni jambo la kheri na nibudi kuwa hai kwani kunawafanya watu kuwa karibu na jamii kwa kujitoa kuwatembelea na    
kuwafariji pia.                                               

     “Tunaishi kwenye jamii nasi pia yatupasa kuwakumbuka wana jamii wanaotuzunguka kwa kujitoa kuwatembelea na kutoa kile kilicho ndani ya uwezo wetu kwa kuwa ni jambo jema na linaleta neema kutoka kwa Mungu  pamoja na kuongeza upendo wa kweli”.Amesema Mbogo
     Pia ameongeza kwa kusema kuwa watoto wanahitaji kufarijiwa ili wasijihisi wanyonge kwa kuwa ni taifa la kesho hivyo kuna ulazima wa kuwa nao karibu zaidi kuwafanya wawe na furaha kila saa kila wakati na wanafarijika wakiwaona wana jamii wakiwatembelea,.
   “Kujitoa kunaleta faraja kwa watoto na   uongozi wa chuo na wanafunzi tumejitolea na miongoni mwa  mahitaji muhimu  tuliyoleta ni pamojana sabuni,maziwa,sukari,luku na unga hivyo ni baadhi tu ambavavyo vinahitajika kwa watoto tunashukuru kwa kuweza kupokelewa na wana Msimbazi”,
     Mlezi wa watoto wa kituo cha watoto yatima cha Msimbazi Center  amewashukuru wanafunzi wa DSJ kwa kuwatembelea na amewataka wazazi wasiwahukumu watoto kwa kuwatelekeza kwa kuwa  ni zawadi kutoka kwa Mungu kupata mtoto.
    Akizungumza na waandishi wa habari kituoni hapo Dada Anna Francis amesema kuwa jamii inabidi itambue thamani mtoto na kumtuza vyema kwani  makosa yamefanywa na wazazi mtoto hana hatia hivyo hapaswi kupewa adhabu ya kutelekezwa na wawe na moyo wa kujitolea kuwatunza.
   “Jamii inabidi itambue makosa ya kutelekeza  yanafanywa na mzazi mwenyewe mtoto hana hatia hivyo yawapasa kuwatuza wakumbuke kwamba wapo wengine wanaomba usiku na mchana wapate  watoto hivyo kuna haja ya kuwatunza vema waige mfano kutoka kwa wanafunzi wa DSJ “.Amesema Francis
    Pia ameongeza kwa kusema kuwa jamii inabidi ikumbuke kujitolea kwa ajili ya kuwasaidia watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu kwani jukumu la kuwalea ni la wana jamii kwa ujumla na kuwachukua watoto endapo watafuata taratibu.
   “Jukumu l a kulea watoto ni letu sote na inaruhusiwa kuwaasili watoto walotimiza miaka mitatu kwa mzazi ama mlezi anayehitaji endapo atafuata utaratibu kwa kupitia ustawi wa jamii na kupewa kibali kama atahitaji kumchukua mtoto wa kumlea ”.
     Sostenes Chuma mwanafunzi wa ngazi ya stashahada amesema kuwa jamii inapaswa ikumbuke kuwatembelea watoto na kujito kuwasaidia kwa kuwa wakifanya hivyo wanawapa faraja watoto ambao wamekosa mapenzi ya wazazi.
    “Inaleta Baraka kutoka kwa Mungu kwa wana jamii ikiwa watajitolea kuwatembelea watoto na watu walio katika mazingira magumu nawasihi waige mfano wa wanafunzi kutoka DSJ watakuwa wamefanya kitu kizuri na chenye maana kwenye jamii”Amesema Chuma
     Nana Mzobora mwanafunzi wa ngazi ya stashahada amesemakuwa anajisikia faraja kuona jamii inasaidia watu walio katika mazingira magumu na kuwasihi kuwa na moyo huo kwa kuwa jamii inahitaji ushirikiano na kuwasihi wasichoke kujitoa.
   
Wanafunzi wa DSJ wamekuwa na utaratibu wa kuwatembelea wana jamii wanaohitaji kutembelewa ikiwa ni sehemu ya kujumuika na jamii kwa kuwa wanatambua thamani ya ushirikiano na wamekuwa wakishirikiana kwenye masuala muhimu

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad