SIMBA WATAKATA KWA MKAPA WASHINDA MBELE YA ASEC MIMOSAS - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Sunday, 13 February 2022

SIMBA WATAKATA KWA MKAPA WASHINDA MBELE YA ASEC MIMOSAS

 

WAPAMBANAJI katika Kombe la Shirikisho, Simba leo Februari 13 wameibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast.

 Ushindi huo unawafanya waongoze kundi wakuiwa na pointi tatu na mabao matatu kibindoni na wamefungwa bao moja.

Bao la mapema lilijazwa kimiani na Pape Sakho ilikuwa dakika ya 12 kwa pasi ya Shomari Kapombe lilidumu mpaka muda wa mapumziko.

Kipindi cha pili ASEC Mimosas walifanya kweli na kupata bao la kusawazisha dakika ya 60 kupitia kwa Aziz Stephan ambaye alitumia vema makosa ya safu ya ulinzi wa Simba chini ya Joash Onyango.

Bao la pili kwa Simba lilipachikwa na Kapombe ambaye alifunga kwa mkwaju wa penalti moja matata ilikuwa dakika ya 78.

Iliwachukua dakika tatu mbele Simba kupachika bao la tatu kupitia kwa Peter Banda ambaye alionyeshwa kadi ya njano kutokana na kuvua jezi wakati anashangilia.

Licha ya ushindi huo ASEC Mimosas walionekana wazuri katika umiliki na waliweza kufanya hivyo kwa asilimia 52 huku Simba ikiwa ni asilimia 48.

 Mchezo wao wa marudio unatarajiwa kuchezwa Machi 20 nchini Ivory Coast hivyo Simba bado wana safari ndefu katika kundi D katika Kombe la Shirikisho.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad