KIKOSI cha Simba kwenye mechi mbili mfululizo za kirafiki safu yake ya ushambuliaji haijafunga na ile ya ulinzi imetunguliwa bao mojamoja kila mchezo.
Kituo kinachofuata ni dhidi ya KMC kisha kimataifa dhidi ya Big Bullets.
Kocha Zoran Maki amabainisha wazi kuwa kuna jambo ambalo linawasumbua washambuliaji wake hivyo anakwenda kulifanyia kazi.
"Haina maana kwamba hatupati nafasi, washambuliaji wanashindwa kumalizia kile ambacho kinatengenezwa tutafanyia kazi kwenye mechi zijazo.
"Tunaamini kwamba kila mchezaji anatambua kaziyake na tutakwenda kufanyia kazi makosa yetu ambayo tumefanya,".
Mechi za Simba: Al Hilal 1-0 Simba, Simba 0-1 Arta Solar, zote za kirafiki.

No comments:
Post a Comment