KIKOSI cha Azam FC kimeambulia pointi moja kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Yanga wakiwa ugenini kwa mara ya kwanza ndani ya ligi.
Mechi mbili ambazo Azam ilicheza ilikuwa Uwanja wa Azam Complex iliambulia sare moja na ushindi mchezo mmoja hivyo leo inakuwa ni sare ya pili.
Azam FC Ikiwa chini ya Kali Ongala, ambaye ni kocha wa washambuliaji walianza kupachika bao la kuongoza kupitia kwa Daniel Amoah dakika ya 25 kisha Yanga wakafunga bao la kusawazisha kupitia kwa Feisal Salum dakika ya 57.

No comments:
Post a Comment