ZILIKUWA DAKIKA 180 ZA KIVUMBI NA JASHO - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Saturday 3 February 2024

ZILIKUWA DAKIKA 180 ZA KIVUMBI NA JASHO

 


KIVUMBI cha msako wa bingwa mpya wa Azam Sports Federation kinaendelea ambapo katika raundi ya pili wababe walikuwa kazini kila timu kusaka ushindi.

Kagera Sugar waliibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Dar City ambao wameumaliza mwendo. Katika ardhi ya Dar vigogo wawili walikuwa kazini wakiandika rekodi namna hii:-

Hat trick hii hapa

Mwamba Clement Mzize mshambuliaji wa Yanga alifunga hat trick kwenye mchezo wa raundi ya pili dhidi ya Hausing kwenye mchezo huo alifunga mabao hayo kipindi cha kwanza alifunga mabao mawili na kile cha kwanza bao moja.

Ni dakika ya 26, 32 na 35 mwamba huyo alifunga huku mfunguzi wa bao la kwanza akiwa ni kiungo Jonas Mkude dakika ya 19 na lile la pili lilifungwa na Skudu Makudubela dakika ya 25.

Mabao 10 yakusanywa

Ndani ya dakika 180 kwenye mechi mbili tofauti ni mabao 10 yalikusanywa raundi ya pili katika Uwanja wa Azam Complex uliotumika na vigogo wa Dar.

Walianza mabingwa watetezi Yanga waliotwaa ubingwa wa Azam Sports Federation kwa ushindi dhidi ya Azam FC 2023 ambapo walipata bao 1-0 lililofungwa na Kennedy Musonda Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Kwenye mchezo wa Yanga ni mabao sita yalikusanywa ambapo Yanga 5-1 Hausing FC ya kutoka Njombe. Bao la Hausing lilifungwa dakika ya 69 na nyota Tony Jailos ambaye alitoka kuwafunga Mgororo ya Mufindi mabao mawili kwenye mchezo wao uliopita.

Mchezo wa pili ulikuwa ni Januri 31 ambapo ubao wa Uwanja wa Azam Complex ulisoma Simba 4-0 Tembo.

Wapya kazini

Nyota Shekhan Khamis alikuwa miongoni mwa nyota waliokuwa kwenye mchezo dhidi ya Hausing na alipiga shuti ambalo halikulenga lango dakika ya 85 huku Joseph Guede akitambulishwa kwenye mchezo huo.

Kwa upande wa Simba ni Michael Fred alianza kikosi cha kwanza na alitoa pasi ya bao dakika ya 11 kwa Luis Miquissone, Pa Jobe alitokea benchi alifunga bao dakika ya 83 na Saleh Karabaka naye alianzia benchi alifunga bao dakika ya 81.

Edwin Balua na Ladack Chasambi walipata nafasi ya kuonyesha uwezo wao kwenye mchezo huo awa funga Januari 31.

Ntibanzokiza katika ubora

Kwenye mabao manne ambayo yalifungwa na Simba Saido Ntibanzokiza alikuwa kwenye ubora wake alipohusikakatika mabao matatu, alitoa pasi mbili za mabao na kufunga bao moja kwenye mchezo huo.

Makipa kazini

Kipa wa Yanga, Aboutwalib Mshery alifungwa bao moja dhidi ya Hausing ambao walipiga jumla ya mashuti mawili yaliyolenga lango huku Hussein Abel aliyeanza langoni kwenye mchezo dhidi ya Simba yeye hakufungwa.

Kadi za njano

Nyota wawili wa Hausing walionyeshwa kadi za njano ilikuwa dakika ya 75 Prince Anthony na dakika ya 76 Elia Lazaro huku kwenye mchezo wa Simba dhidi ya Tembo beki Shomari Kapombe alionyeshwa kadi ya njano dakika ya 76.

 Bao la mapema

Azam Complex ilishuhudia bao la mapema likifungwa dakika ya 11 na mtupiaji alikuwa ni Luis huku lile la jioni pia likifungwa na Pa Jobe dakika ya 83.

 

 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad