UONGOZI wa Cosmopolitan umebainisha kuwa mpango mkubwa ni kupata pointi tatu muhimu kwenye mchezo wa Championship dhidi ya wapinzani wao Pan Africans wakiwa ugenini.
Mchezo huo
unatarajiwa kuchezwa leo Februari 3 Uwanja wa Mabatini, Pwani kwa wababe hawa
wawili kusaka pointi nani ya dakika 90.
Ikumbukwe
kwamba Ofisa Habari wa Cosmopolitan, Leen Essau aliibuka ndani ya timu hiyo
akitokea Pan Africans hivyo mbali na ndani ya uwanja kuwa na vita ya msako wa
ushindi nje ya uwanja viongozi wanatambua kwa uzuri.
Leen aMEsema kuwa maandalizi yapo vizuri na wapo tayari
kwa mchezo huo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.
“Ni mzunguko
wa pili kwetu kwa kuwa wanakumbuka mchezo wa kwanza tukiwa nyumbani tulishinda
bao 1-0 na sasa tunawafuata ugenini kupata pointi tatu muhimu mashabiki
wajitokeze kwa wingi kushuhudia burudani, “ alisema Leen.
Cosmopolitan
ipo nafasi ya 11 ikiwa na pointi 18 inakutana na Pan Africans iliyo nafasi ya
14 na pointi 15.
No comments:
Post a Comment