AZAM FC KAZI INAENDELEA - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Thursday, 11 November 2021

AZAM FC KAZI INAENDELEA

 


WACHEZAJI wa Azam FC wameendelea na maandalizi ya mechi zao zijazo za Ligi Kuu Bara na chimbo lao likiwa ni palepale katika Uwanja wa Azam Complex. 


Timu hiyo chini ya Kocha Mkuu, George Lwandamina katika mechi tano ambazo ni dakika 450 imekusanya pointi 7 ipo nafasi ya nane na safu yake ya ushambuliaji imetupia mabao manne.


Katika kujiweka sawa zaidi inatarajia kushuka uwanjani kwa mara nyingine tena Novemba 13 itakuwa dhidi ya JKU SC kutoka Zanzibar. 


Mchezo huo utakuwa ni wa kirafiki kwa muda huu ambao ligi imesimama kupisha maandalizi ya timu ya taifa kushiriki mechi za kufuzu Kombe la Dunia, 2022 Qatar.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad