MECHI ya kirafiki imekamilika Uwanja wa Azam Complex leo 30 ambapo Yanga imeibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mafunzo FC.
Mabao yamefungwa na Mapinduzi Balama dk ya 19 Heritier Makambo dk ya 52 na lile la ushindi limefungwa na Fiston Mayele dk ya 71 kwa mkwaju wa penalti.
Kwa upande wa Mafunzo FC ni mabao ya Ahmed dk ya 9 na Abdulhakim dk ya 55.
Mafunzo FC walianza kupata bao la kuongoza Yanga wakamaliza kazi kwa kupata bao la ushindi kipindi cha pili.

No comments:
Post a Comment