MAKOCHA wote wawili kwa sasa wanapiga hesabu mara mbilimbili, mechi zao wanazocheza huku wakifikiria na mchezo wa Kariakoo,Dabi Aprili 30.
Ni siku 9
zimebaki kabla ya mchezo huo, hapa tunakuletea baadhi ya nyota wa
kazi kwa Nasreddine Nabi wa Yanga na Pablo Franco wa Simba namna hii:-
Diarra
Djigui
Kipa
namba moja wa Yanga ameanza kikosi cha kwanza mechi 15 na amesepa na dk 1,350
na amefungwa mabao 5 na kakusanya clean sheet kwenye mechi 10.
Katika
mabao hayo ambayo amefungwa hakuna bao alilofungwa kwa mkwaju wa penalti na
lile la kwanza alifungwa na Ruvu Shooting, Uwanja wa Mkapa mtupiaji akiwa ni
Shaban Msala.
Dickson
Job
Job kama
lilivyo jina lake yale yaliyomo yamo ni mtu wa kazi kwelikweli akiwa amecheza
mechi 16 na kutumia dk 1,509 na ana pasi moja ya bao aliyotoa ndani ya ligi.
Yanick
Bangala
Beki wa
kazi ngumu na zile nyepsi akiwa ana uwezo wa kupanda na kushuka ametumia dk
1,431 na ana pasi moja ya bao kati ya 33 ambayo yamefungwa na timu hiyo.
Said
Ntibanzokiza
Wamanuita
‘Father’ wa Yanga akiwa ni kiungo mwenye uzoefu mkubwa na soka la ushindani na
amecheza mechi 12 katupia mabao 6 na ana pasi nne za mabao kayeyusha dk 1,048.
Feisal
Salum
Mechi 16
kacheza ndani ya Yanga akiwa ameyeyusha dk 1,325 katupia mabao 4 na pasi 3 za
mabao,kazi kubwa ni kwenye kutibua mipango ya wapinzani na kutengeneza nafasi.
Fiston
Mayele
Namba
moja kwa utupiaji akiwa na mabao 11 na pasi 3 za mabao. Kacheza mechi 19 na
kusepa na dk 1,475.
Djuma
Shaban
Mechi
zake ni 16 na amefunga mabao 3 na pasi 3 huku akiwa kasepa na dk 1,437.
Simba
Aishi
Manula
Air
Manula kwenye himaya yake kaka langoni kwenye mechi 16 kafungwa mabao 7 akiwa
naclean sheet 9 na n idk 1,440 kazitumia uwanjani.
Mechi
yake ya kwanza kufungwa ilikuwa dhidi ya Ruvu Shooting na ni Elias Maguli
alimuachia ganzi kwenye mikono yake kwa msimu wa 2021/22.
Henock
Inonga
Kazi
chafu zinaanza hapa kwenye eneo la kati katika mechi 13 ambazo kacheza ni dk
1,055 huku akiwa sio mtu mzuri ikiwa utamzingua kwa kuwa kutembeza vichwa kwake
sio jambo gumu japo sio mchezo wa kiungwana kama alivyofanya mbele ya Coastal
Union na kuonyeshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja.
Sadio
Kanoute
Mtaalamu
wa mipira mirefu na mguso wake ni mara moja tu.Kiungo huyo amecheza jumla ya
mechi 8 na kusepa na dk 668.
Katupia
bao moja kwa kutumia kichwa akiwa ndani ya 18 na bado hajatoa pasi ya bao.
Bernard
Morrison
Mzee wa
kuchetua katumia dk 645 na amefunga bao moja na kutoa pasi mbili za mabao
akiwapa washkaji zake Meddie Kagere na Mzamiru Yassin akiwa amecheza mechi 11.
Shomari
Kapombe
Ili ukuta
wa Pablo ukamilike utamkuta Kapombe mwenye pasi mbili na kutumia dk 1,24.
Meddie
Kagere
Kwenye
upande wa ushambuliaji kifaru hiki kutoka Rwanda ni namba moja na kimetupia
mabao 7 na pasi moja ya bao.
Jonas
Mkude
Mkongwe
mwenye ujuzi mkubwa akiwa yupo kwenye ubora uleule kwa muda wa zaidi ya miaka
10, mpe kazi ya kucheza na mpira lazima utakubali kazi yake akiwa ametoa pasi
mbili za mabao.
No comments:
Post a Comment