UONGOZI wa Yanga umeweka wazi kuwa beki wao wa kazi ngumu Djuma Shaban hali yake kwa sasa inaendelea vema baada ya kupata maumivu hivi karibuni.
Djuma hakuwa sehemu ya kikosi kilichopoteza kwa kufungwa mabao
2-1 dhidi ya Ihefu mchezo uliochezwa Uwanja wa Highland Estate ambapo rekodi ya
Yanga kutofungwa mechi 49 iligotea hapo mazima.
Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe amesema kuwa maendeleo ya
nyota huyo kwa sasa yanaendelea vizuri kwa mujibu wa ripoti za madaktari.
“Hali ya Djuma kwa sasa inaendelea vizuri jambo ambalo
tunamshukuru Mungu kwa hili na tunaamini kwamba atarejea uwanjani kuendelea na
majukumu yae.
“Hata Farid Mussa naye hakuwepo kutokana na kuwa na matatizo ya
kifamilia.Kuhusu mipango yetu kila kitu kinakwenda sawa na tunaamini kwa mechi
zetu tutapata matokeo chanya,”.
Djuma ni mechi 8 kacheza akiyeyusha dakika 520 kafunga bao moja na pasi moja ya bao alikuwa sehemu ya kikosi kilichoshinda bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons, Uwanja wa Mkapa.

No comments:
Post a Comment