ILE simulizi ya Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo iliyokuwa ikiandikwa gazeti la Championi Jumatano visa vyake viliandikwa kwenye mikoa zaidi ya miwili Tanzania kwa lengo la kufikisha ujumbe kwa jamii husika.
Ipo wazi kwamba simulizi ya Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo
inaingia kwenye orodha ya simulizi bora zilizopata nafasi ya kuchapishwa ndani
ya gazeti la Championi Jumatano ikiwa ni utunzi wa Lunyamadzo Mlyuka.
Kwa sasa mchakato unaendelea kufanyia kazi maombi ya wasomaji
kupatikana kitabu kinachotarajiwa kutoka hivi karibuni na oda kutoka sehemu
mbalimbali zimeanza kutolewa ikiwa ni pamoja na Lindi, Njombe, Kibaha, Arusha, kuna
nafasi ya kutoa oda pamoja na udhamini.
Akizungumza kuhusu mikoa iliyopata nafasi ya simulizi hiyo
kuandikwa kwa nyakati tofauti na visa vikapatikana, Mlyuka alisema: “Kuna
sehemu mbalimbali ambazo zimejumuishwa ndani ya simulizi ya Ganzi ya Maumivu
Kwenye Upendo ikiwa ni Mtwara, Kibaha, Arusha, Iringa, Njombe kwa lengo la
kuongeza ladha na simulizi kuwa kwenye ubora wake.
“Ina visa vingi vya kuvutia na kusisimua hivyo sio kazi ya kuikosa
kwa kuwa inatoa elimu kuhusu maisha halisi tuliyopo kwa sasa, furaha, huzuni
yale yote yanayoifanya dunia izunguke yapo kwenye simulizi ya Ganzi ya Maumivu
Kwenye Upendo,”.
Kwa oda, udhamini wasiliana moja kwa moja na mwandishi 0756 028
371. Kwa sasa simulizi inayoendelea ni Msichana wa Maisha Yangu, ndani ya
Championi Jumatano.

No comments:
Post a Comment