GAMONDI AWAPA TANO WACHEZAJI ISHU YA 5G - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Wednesday 21 February 2024

GAMONDI AWAPA TANO WACHEZAJI ISHU YA 5G

 


MIGUEL Gamondi, Kocha Mkuu wa Yanga amesema wachezaji wamejituma na kutimiza majukumu yao ndani ya uwanja mbele ya Polisi Tanzania.

Ipo wazi kwamba Yanga ni mabingwa watetezi wa Kombe la Azam Sports Federation walipata ushindi kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Azam FC mchezo uliochezwa Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Februari 20 ubao wa Uwanja wa Azam Complex ulisoma Yanga 5-0 Polisi Tanzania na mabao yakifungwa na Joseph Guede aliyefunga mabao mawili dakika ya 13 na 45 huku Farid Mussa dakika ya 33 akipachika bao moja, Clement Mzize alipachika bao moja dakika ya 82 na kamba ya tano ni mali ya Shekhan Khamis dakika ya 86 kwa penalti.

Nyota Guede na Okra kwenye mchezo huo walifanya kazi kubwa kwa kushirikiana na wachezaji wengine kufunga na kutoa pasi za mabao ambayo kazi hiyo ilifanywa na Okra.

Gamond amesema: "Wachezaji wamejituma kwenye kutimiza majukumu yao katika hilo tunapawa pongezi na tunaamini kwamba kazi bado inaendelea kwa ajili ya mechi zijazo,'.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad