KIUNGO mshambuliaji wa Yanga SC, Clatous Chama anatajwa kuwa kwenye rada za Klabu ya Zesco United ya Zambia.
Chama ambaye alitambulishwa rasmi Yanga SC Julai Mosi 2024, mkataba wake wa mwaka mmoja umeggota mwisho.
Alitambulishwa hapo akiwa mchezaji huru akitokea kikosi cha Simba SC ambacho kimegotea nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.
Taarifa zinaeleza kuwa mazungumzo ya wakala wa Chama na Zesco United yamefikia kwenye hatua nzuri kilichobaki nyota huyo kusaini na kutambulishwa ikiwa mabosi wa Yanga SC watamchunia moja kwa moja.
Yanga SC wanatambua mkataba wa mchezaji huyo umeisha na hawajafanya mazungumzo yoyote jambo linaloashiria kwamba ni asilimia kubwa hatakuwa kwenye ligi namba nne kwa ubora Afrika Clatous Chama msimu wa 2025/26.
Msimu wa 2024/25, Chama alifunga mabao sita na katika mabao hayo mabao mawili alifunga kwa mapigo huru akiwa nje ya 18.
Imeandikwa
na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo,
kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya
Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa
Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa
Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo
Wangu Unavuja Damu itazinduliwa rasmi Julai 24 2025 usipange kukosa.
No comments:
Post a Comment