Homa ya Mtihani yasumbua DSJ - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Wednesday, 2 November 2016

Homa ya Mtihani yasumbua DSJ

WANAFUNZI wa chuo cha uandishi wa habari Dar es Salaam
wameuomba uongozi wa chuo kuwapa namba za maomo ili waweze kusoma ratiba ya mtihani kwa umakini na kuelewa masomo watakayoanza nayo kwenye mitihani

Wanfunzi wa DSJ wakiwa kwenye mabenchi wakijisomea 
Zainabu Hamisi mwanafunzi wa ngazi ya stashahada amesema kuwa ratiba inamchanganya kila anapoisoma hali inayomfanya asielewe kipi ni kipi kwenye mpangilio mzima wa ratiba na masomo
watakayofanya.

"Ratiba naiona ila inakuwa ngumu kuielewa maana namba za masomo na mpangilio wa ratiba umekuwa ukinifanya nishindwe kuelewa kipi ni kipi katika namba za masomo na somo lipi litaanza hivyo naomba tupewe namba za masomo pia".Amesema

Naye Smita Ratan Waziri wa habari na taarifa wa chuo cha DSJ amesema kuwa wamelipokea jambo hilo na wanalifanyia kazi kwa kuwa kazi kubwa ya wizara ni kuhakikisha kuwa wanafunzi wanakuwa na taarifa zinazowahusu

"Tunatambua wajibu wa wanafunzi ni kuwa wafuatiliaji nasi jukumu letu ni kuhakikisha tunaweza kuwapa taarifa sahihi na kwa wakati sahihi zaidi hivyo naamini utekelezaji tu ndio umebaki wasiwe na wasiwasi kila kitu kitakuwa sawa".Amesema

Wanafunzi wa chhuo cha uandishi wa habari DSJ wapo kwenye maandalizi ya kuelekea kufanya mitihani yao kwa ajili ya kumalizia muhula wa masomo kwa mwaka 2016 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad