MTANGAZAJI wa luniga
ya clouds katika kipindi cha 360 Samweli
Nathanaeli amewataka waandishi wa habari kutokukata tamaa mapema katika
kupambana na harakati za kutafuta ajira pamoja
na changamoto zinazotokana na maendeleo ya sayansi na technolojia.
Nathanaeli amesema kuwa tasnia ina mambo mengi hivyo kuna
umuhimu wa wanahabari kuwa na uvumilivu na kujituma kwa juhudi ili na kuwa
wabunifu zaidi kwa kuendana na technolojia na jambo la muhimu kwa waandishi ni
kutumikia kwa wanajamii.
| Nathaniel Smweli akiwafunda wanahabari waliohudhuria semina iliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi Basata |
“Uwepo wa mitandao ya kijamii kama facebook , istagrasm
,twiter unafanya wana jamii kuwa na imani zaidi kwa mitandao ya kijamii na
tukio lolote likitokea kila mmoja anafanya kazi ya kuripoti
matukio kama
mwandishi wa habari”. Amesema
Aidha ameongeza kwa kusema kuwa mwandishi anajukumu la
kujikubali mwenyewe na asihisi kuwa hana uwezo wa kufanya vizuri katika tasnia
ya habari na mazingira yasiwe chanzo cha kushindwa kufanya vizuri zaidi.
“Kuna umuhimu wa kujikubali na kujituma kwa kufanya kazi na
sio kujikatisha tamaa na kuhakikisha unaweza kufanya mambo kwa mpangilio na
kuwa kiraka kwa kuweza kufanya kazi zaidi ya moja katika tasnia ya uandishi na
utangazaji pia”.Amesema
Zainabu Nassoro ambaye ni mwandishi wa habari amesema kuwa
kuna umuhimu wa kujituma na kupambana na changamoto za maendeleo ya technolojia
kwa kuwa ni kitu kisichoweza kuzuilika kirahisi.
“Hakuna anayeweza kuzuia maendeleo ya teknolojia hivyo kuna
haja ya kutambua ni namna gani tunaweza kuzishinda na kuendelea kuwa bora zaidi
katika kazi yetu ya kufikisha taarifa kwa jamii inayotuzunguka”.Amesema
No comments:
Post a Comment