Utunzaji mazingira bado msamiati - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Tuesday, 1 November 2016

Utunzaji mazingira bado msamiati

                                        
KIMYA kilitawala kwa muda usiopungua dakika tatu mara baada ya kutokea sauti ya kishindo kikubwa kutoka maeneo yaliyo karibu kabisa na makazi ya watu hali iliyofanya kila mmoja kuacha shughuli aliyokuwa akiifanya.

Mazingira yetu tuyatunze na kuyalinda pia
Wote wakawa wanajiuliza nini hicho kwanini iwe hivyo na mwanzilishi wa haya mambo ni nani maswali yote yalitoka bila kuwa na majibu sahihi kwa muda ule kwa wana jamii katika maeneo ya mtaa wa saba .

Nisizame ndo ikawa sauti ya kwanza kuweza kusikika na kusema kwa nguvu kuwa mambo yanazidi kuwa magumu ,kutahamaki kila mmoja anashika njia yake baada ya kusikia mlio wa king’ora cha
gari ya polisi kikielekea eneo la tukio.

Kila mmoja ana uhitaji mkubwa kuishi katika mazingira mazuri na kuwa na vitu vizuri vynye thamani zaidi ya mwenzake namna ya kuipata na kumiliki hivyo ndipo kunakuwa na utata mkubwa kwa wale wanaoishi kwenye mazingira kutumia.

Njia iliyo rafiki kabisa ni kuhakikisha kuwa hakuna anayepoteza muda na nguvu kuwekeza na kufanya jambo litakalomuumiza yeye na familia yake pia kwa ujumla umakini unahitajika katika kutekeleza majukumu ya kujenga taifa.

Mazingira yetu ambayo tunaishi yana mambo mengi na shughuli nyingi zinazofanyika zinategemea uwepo  wa mazingira ili kufanikisha mipango ya binadamu walio chini ya sayari ya sayari ya tatu ambayo ni dunia

Kila siku miti inakatwa na hakuna anayejali kuhusiana na uwepo wa misitu hiyo wala kushughulika na kufuatilia masuala ya upandaji wa miti baada ya kukata miti katika maeneo mbali mbali nchini yenye hifadhi ya misitu.

Kuna haja ya kutunza mazingira yetu kwa kuhakikisha kuwa taratibu na sheria zinafuatwa kwa watu wote kwa kuwa kila kiumbe kinategemea kuishi na kufanya mipango yote kwenye mazingira tunayoishi.

Aidha serikali iweke mipango rafiki kwa wananchi wake ili kuweza kuwa ni shirikishi kwa wtu wake na kuhakikisha kuwa ukataji wa miti kiholela na utupwaji wa taka maeneo yasiyo rasmi unathibitiwa pamoja na kuweka sehemu maalumu za kutupia taka.


Mazingira yakitunzwa vema yanaleta raha na faraja kwa wale wanayoyaona na pia kwa manufaa ya kizazi kijacho ambacho nacho kinahitaji kujengewa mazingira mazuri zaidi kwa kuwa hakuna anayependa kuishi kwenye mazingira yasiyo na mvuto.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad