Hayo yamesemwa Rahim Mwanga Afisa masoko na uhusiano wa UTT AMIS (Taasisi ya serikali iliyo
chini ya Wizara ya Fedha) iliyopo mtaa wa Sokoine na Ohio Dar es Salaam
alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Kibaha mkoani Pwani
alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Kibaha mkoani Pwani
“Hatushauri wananchi
kukopa ila tunawashauri kutafuta mitaji ili waweze kupata faida zaidi kwani
mikopo ikizidi inaleta umaskini na kama wanahitaji mikopo,mkopo mzuri ni ule
unaowekezwa katika uzalishaji ili upate fedha za kulipa huo mkopo”alisisitiza
Mwanga.
Aidha aliongeza kwa
kusema kuwa kwa mwananchi yoyote anayayetaka kuwekeza sehemu yoyote ile ni vema
kutafuta ufahamu na ushauri kutoka kwa wataalamu juu ya masuala ya uwekezaji ila maamuzi yanabaki
kwa mwananchi mwenyewe.
“Watumieni wataalamu wa
masuala ya uwekezaji ili kujua kama sehemu utakayowekeza utapata faida au
hasara kwani hakuna mwekezaji anayefikiria kupata hasara hivyo ni muhimu
kutafuta ushauri kwani ni bure kabisa” alisema.
Naye Afisa masoko wa UTT
AMIS Waziri Ramadhan amewataka wananchi kuitumia taasisi hii kama kiunganishi
katika uwekezaji ili waweze kutimiza malengo yao kwani mfuko huo unamjali kila
mmoja bila kuwa na ubaguzi wowote ule.
UTT AMIS iliazishwa
mwaka 2008 inasimamia mifuko zaidi
ya mitano mpaka sasa ambayo ni pamoja na mfuko wa umoja,wekeza maisha,mfuko wa
watoto,mfuko wa kujikimu na ukwasi na ni kwa watu wote.

No comments:
Post a Comment