Harakati za mtu mweusi hazina mwisho wala mwanzo kwani tangu
alipoletwa duniani alikuta wazazi wake wapo katika harakati nay eye alipokuwa
akajikuta yupo ndani ya harakati.Mchana hata usiku bado pilika pilika
zinaendelea kwa mwanaharakati ikitokea ukapata bahati ya kunmuuliza kulikoni
mbona hivyo atakujibu kwa wepesi kabisa tena huku akicheka na kufuta jasho kwa
kiganja cha
mkono na kukwambia si unajua tena mambo mengi.
mkono na kukwambia si unajua tena mambo mengi.
Hapo ndipo utakapopigwa ganzi baada ya muda mfupi kupita
yuleyule aliyekwambia mambo mengi kumkuta sehemu za starehe tena katika hali ile ile si jambo la kumshangaa bado
utapenda kujua tatitizo ni nini utamfuata na kumuuliza swali lile lile kulikoni
mbona hivyo hapo sasa namna ya kukujibu itakuwa tofauti lazima anyanyue chupa
yenye kinywaji baada ya muda atakwambia napunguza mawazo nawe huna budi
kuondoka.
Kutahamaki unakutana
naye tena barabarani akiwa peke yake na shati kaweka begani akibadilisha lugha
za kigeni kama msomi wa chuo kikuu huku akitoa lugha zisizo eleweka kwa watu
walio karibu naye akiwataka wasimpe msaada tena kwani yeye anauwezo wa kifedha
na ni msomi pia bado una nia ya kutka kutmbua tatizo nini naye atkuongelea
lugha anayoyoijua yeye mwenyewe kasha atakwambia neon fupi litakalokuacha njia
panda yani we acha tu atatikisa kicha na kuendelea kuongea lugha za kigeni’
Umefika nyumbani unaendelea kutathmini majibu uliyoambiwa na
mwanaharakati mara unaskia kelele mamaaa nakufaaa jamani nisaidieni unakurupuka
na kutoka nje kutambua sauti inatokea wapi unagundua kuwa ni kwa mwana harakati
yuleyule unayemfkiria unaongeza spidi ili ufike eneo la tukio ili usingoje
kusimuliwa unany’ong’onyea kabisa kwani mwanaharakati anamshushia kipigo mke
wake kisa amechelewa kufungua mlago unapouliza kulikoni utaskia haya maisha tu.
Sasa hapo ndipo utakapokuwa umepata majibu ya maswali yako
tangu pale awali mpaka mwisho kumbe harakati zote zile za mwanaharakati
kujituma katika kazi usiku na mchana kwenda sehemu za starehe kufanya mambo
yake bila mke wake kuongea lugha za
kigeni mithili ya kasuku na kuto hitaji msaada kwa rafikize na mwisho kumpiga
kipenzi cha moyo wake kwa kosa la kwake mwenyewe ndio maana halisi ya neno maisha.
Kwa maana hiyo maisha yanaanza tangu ile siku unayoletwa
duniani na kadri unavyozidi kukua ndivyo unavyozidi kuwa mwanaharakati kwa
kufuata nyayo za wale waliokutangulia kama ndo hivyo mpaka hapo kuna haja ya
wale waliokutangulia na wle unaowafuata nyayo zao kukupa wewe mbinu mbadala ili
uepuke yale ambayo wao wameyafanya na baadae kuwaingiza katika matatizo kama
mwanaharakati.
Maisha yanahitaji umakini mkubwa katika kila hatua
unayopitia haijalishi upo wakati gani uwe wakati wa kucheka ama wakati wa kulia
bado unatakiwa kuwa makini ili uweze kuvuka katika hatua hiyo salama salmini
achana na ile kasumba ya kufikiria kulala maskini na kuamka tajiiri hizo ni
ndoto za Abunuwas ambaye hata yeye zilimshinda kuziota akaamua kuamka kuendelea
na shughuli nyingine.
Kukurupuka na kufanya maamuzi katika maisha kutakufanya
upoteze dira na kuanza kuyumba mithili ya Ngoswe hali itakayokufanya upoteze na
kushusha hadhi yako katika jamii jichunge katika kila hali na kila jambo
unalolifanya itengeneze leo vizuri ili iwe rahisi kwa wale watakaokufuat kesho’
Maisha ni kitu ambacho kipo kwa kuwa ulikikuta pia utakiacha
kwa kuwa hakina tatizo na wewe hakuna mwenye hisa na maisha hata uwe mjanja
kiasi gani maisha bado yanakusomea ramani hivyo kuwa makini acha kukurupuka
jipange fanya mambo yako kwa umakini wa hali ya juu kila kitu kwako kitakuwa
sawa kwa manufaa yako na jamii kwa ujumla.
Malengo ambayo ni sawa na ilani yako usiyapuuze hata kidogo
kwani adui wa kwanza katika maisha ni nafsi yako mwenyewe,ndio ni nafsi yako
mwenyewe hebu jiulize swli hili ni mara
ngapi umeiambia nafsi yako kuwa utafanya jambo flani labda kama ni
kuacha pombe au kwa mwanafunzi kusoma sana baada ya kufeli mwisho wa siku kila
kitu kinabaki vile vile kikielea bila utendaji wowote je katika hili nani ni
adui?
Yote kwa yote kuna changamoto kubwa sana katika gharama za
maisha kadri siku zinavyozidi kwenda ndivyo hali ya gharama za maisha na uchumi
vinazidi kupanda bila kujua chanzo ni nini na kitu cha kushangaza tunapewa
ripoti kwa namba kuwa eti uchumi wa taifa umepanda kwa asilimia hapo ndipo
nakumbuka kauli ya mwanaharakati inayosema yani we acha tu,haya ndo maisha
yaliyojaa visa na mikasa maumivu na furaha pia.
Tabia za watu huwezi kuzitabiri hata kidogo katika safari ya
maisha kwani Yule unayemwamini na kumthamini huenda haitambui thamani yako hata
chembe ila yupo nawe kwa sababu unanguvu katika kusukuma gurudumu la maisha
lengo lake akifika sehemu anayokusudia aendelee na safari yake bila uwepo wako
inaleta huzuni na simanzi pia kwani kumuamini mtu ni sawa na kuwekeza ili
baadaye muweze kupata faida pamoja.
Hata uwe komandoo katika hilo lzima litkugusa na kukupa
wakati mgumu pia hauna jinsi kwani tumekwisha kutambua kuwa maisha hayana shida
na wewe kwa kuwa uliyakuta hata ukiondo tukikusindikiza tutaumia tukirejea
tushakusahau na tunaendelea kuparaganyika na harakati zetu pamoja na zile
ulizoziacha pia tutaziendeleza kwa kuwa nasi maisha hayana shida na sisi
tuliyakuta pia.
Hali ya kukata tama mapema na kuhisi kuwa hakuna njia
nyingine ya kufanya ili uweze kufanikiwa huo ni uvivu wa kufikiria ndio maana
siri nyingi zilizowekwa kwenye vitabu bado ni gumzo kwa mwanaharakati hajapata
muda wa kuzisoma bado anaendelea na harakati za kutafuta maisha kasha baadaye
akapunguze mawazo sijui ni mawazo gani hayo yanayopunguzwa kwa mtindo huu wa
kisasa kabisa.
Zama za mababu zetu mawazo yalipunguzwa kwa mtindo wa
kipekee mathalani kwa mtoto wa kikulima akiwa na mawazo anachofikiria daima
huwa ni kulima tu hivyo akipata hilo wazo ataelekea shambani na kulianda shamba
kama si msimu wa kulima na kuanza kulima kama ni msimu wa kulima,Wamasai wao
wnawaza kuwinda tu ili kuonesha ushupavu na uhodari wakianza kuwaza tu hao
porini kuwinda samba ,cha ajabu karne hii kila anayewaza utaskia nataka chupa
bora umpe maji ili kushusha presha.
Hakuna tunzo katika kusababisha maumivu kwa mtu mwingine
zaidi ya nafsi yako kukusuta ila maisha hayahitaji kulipza kisasi wala kuwa na
kinyongo na mtu mwaingine kwani kila mtu anatembea na funguo za mafanikio za
mtu asiyemjua watakutana wpi na lini ili aweze kumpa hiyo funguo yake ya
mafanikio yatupasa kuwa na upendo kwa wote ili tuweze kufikia malengo na kuwa
wanaharakati wa kujitegemea na sio tegemezi.
Yoyote anayekaribishwa na kuingia katika harakati ni sawa na
mtu aliyewekwa katika chumba chenye giza na hatambui sehemu ilipo tochi au
kiberiti ili aweze kuwasha na kupata mwanga hata apige yowe namna gani giza
halitaondoka kwa kuwa hakuna kitendo kinachofanyika zaidi ya kuwa na wazo tu la
kuhitaji mwanga maisha yanahitaji wazo na kitendo pia ili kile unachokifikiria
kiweze kutokea.
No comments:
Post a Comment