| Elimu bure imefungua mwamko wa wa wazazi kupeleka watoto shule kuongeza ujuzi |
HAKUNA marefu yasiyo na ncha ni msemo ulioachwa na mababu
zetu nina imani walikuwa wametulia chini ya mwarobaini wakinywa kahawa na
kuleta hadithi za hapa na pale baada ya
kumaliza kufanya kazi zao na mihangaiko
ya hapa na pale.
Imani yao ilikuwa ikiwatuma kuwa kila wakati wa kutenda
jambo kuna ulazima wa kufikiria na kutazama uwepo wa kesho na na kujipanga
zaidi pale unapokwama ili uweze kufikia
malengo ni muhimu kutambua aina zote na kujitoa kwa hali na mali.
Si wote wanaotambua thamani ya muda utata mkubwa unakuja
pale ambapo unakuwa umebakiwa na muda wa kawaida tu kufanya mambo mengi na
makubwa hapo ndipo pumzi inaposhuka na kudhani kuwa upo dunia nyingine.
Ndugu zetu wameanza kuhitimisha safari yao ya miaka mine ya
masomo baada ya mapambano yote ya siku na miaka kadhaa kwenda na kurudi
nyumbani na wengine walikuwa wakiishi shuleni wapo waliokuwa wakikaa kwa
marafiki.
Neno mtihani lina mitihani mingi na ni msamiati ambao ukiutaja
kwa mwanaharakati yeyote lazima atapigwa ganzi na kukupa maana ambayo yeye
mwenyewe anaitambua na anaielewa kwa mujibu wa uelewa wake.
Abdalah Ally miongoni mwa wanafunzi anasema kuwa anapenda
sana kusoma na kujifunza mara kwa mara na siku zote anahakikisha kuwa ana kitu
kipya kakipata na kuongeza katika ubongo wake na kwa watu wake a karibu.
“Najifunza siku zote kitu kipya na huwa nawashirikisha na
ndugu zangu na jamaa niwapo shule juu ya umuhimu wa kujifunza mambo mapya kila
siku bila kujali nipo katika mazingira gani na wakati pia ni jambo la
kuzingatia”.Amesema
Anafafanua na kusema kuwa
pamoja na kupenda kwake kusoma kuna jambo linalompa wakati mgumu na
linamfanya awe mpweke pindi anaposikia msamiati huo ukipenya kwenye sikio lake
wakti wowote ule.
“Neno mtihani linanipa wakati mgumu na ninashindwa kusema
kuwa naogopa mtihani ila napenda kusoma sipendi kufanya mtihani hasa nyakati za
msimu wa kuelekea na sikukuu huwa zinanipa wakati mgumu “.
Kidato cha nne wanaanza kufanya mitihani yao kwa ajili ya
kuhitimu kidato cha nne na hali hiiinawafanya wawe na ukaribu kabisa na neon
mtihani kwa kuwa wamekuwa watahiniwa ndani ya chumba cha mtihani.
Historia inaandikwa kwa mara ya kwanza baada ya mchakato
mzima wa serikali ya awamu ya tano kusimamia wanafunzi kupata elimu kwa shule
ya sekondari na msingi bila gharama yoyote ile kwa shule za serikali.
Jamii inaimani na serikali na mpango mzima wa elimu kwa
wanafunzi hivyo kwa kupitia mtihani inakuwa ni kipimo cha kwanza kwa serikali
kutambua kile ilichotengeneza na kuwekeza kwa wanafunzi ambalo ndio taifa la
kesho.
Licha ya changamoto zinazotokea katika sekta ya elimu bado
jukumu la kijifunza na kuboreha mazingira kwa wanafunzi ni letu sote hakuna
anayeweza kulikwepa na kuiachia serikali peke yake suala la kuboresha
miundombinu ya elimu.
Waziri wa wizara ya elimu Joyce Ndalichako amesimama kidete
kuhakikisha kuwa elimu inayotolewa na ujuzi wanaopata wanafunzi ni wenye
kiwango cha hali ya juu utakaoweza kutoa dira nzuri na matokeo mazuri kwa
wanafunzi na wazazi.
Katika hotoba zake rais wa Tanzania amesema kuwa haiwezekani
nchi kama Tanzania wanafunzi kusoma katika mazingira magumu licha ya kuwa na
misitu bado wanaketi chini hili si jambo la kupuuzia na akatoa agizo kwa wakuu
wa mikoa kusimamia upatikanaji wa madawati.
“Kila mkuu wa mkoa ana jukumu la kuhakikisha na kusimamia
upatikanaji wa madawati nawanafunzi wakapata sehemu ya kuketi na sio kuketi
chini na utajiri wa misitu upo nchini hivyo ni wajibu kusimamia na kuhakikisha
tatizo linapungua”.Amesema
Elimu ni jambo la msingi na ujuzi kwa mwanadamu ni zawadi
ambayo hakuna awezaye kuinya’ng’anya pindi inapokuwa imemkaa mtu mwenyewe,kila
la kheri kidato cha nne msichore picha za messi wala Morinyo naamini kila kitu
kitakuwa sawa.
No comments:
Post a Comment