Ukata wawatesa wafanyabiashara - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Tuesday, 1 November 2016

Ukata wawatesa wafanyabiashara

   

Wafanyabiashara wameitaka Serikali kuwapunguzia kodi kwa kuwa hali ya maisha imezidi kuwa ngumu na uchumi unazidi kushuka kwa kasi kila siku kwa wafanyabiashara kutokana na kukosa wateja wa bidhaa mbalimbali.
Wafanyabiashara wakiwajibika  kuwahfunza na kuwahudumia wateja kazini Mkoani Pwani

Akizungumza na mwandishi wetu Hamza Kizogo mfanyabiashara  amesema kuwa hali ya maisha imezidi kuwa ngumu na idadi ya wateja inapungua kila siku kutokana na ukata unaowakabili
watanzania

“Mauzo kwa biashara yangu yameshuka kabisa tofauti na awali kwa kuwa kila siku kunapopampazuka ni afadhali ya jana na bidhaa hasa za matunda zinawahi kuharibika na kusababisha hasara kwa wafanyabiashara”.Amesema

Naye Mama Asha ambaye ni mama lishe amesema kuwa biashara ya chakula imekuwa ikimdodea na wafanyabiashara wengi wamekwama kuendelea na biashara kutokana na ukata unaowakabili.

“Ukata unatumaliza na kutufanya tushindwe kujikimu vema na hali ya kodi inatuumiza kwa kuwa tunaambiwa hapa kazi tu na fedha kwenye mzunguko ni mdogo watu wa chini ndio tunaumia “.Amesema

Naye katibu mkuu wa Mkoa wa Pwani Shangwe Tamala amesema kuwa srikali inatambua changamoto za wafanyabiashara na inajali watu wake hivy utatuzi wa matatizo utafanywa punde,

"Tunatambua uhitaji na matatizo yanayowakibili wafanyabiashara na serikali ya awamu ya tano ni sikivu ipo kwa ajili ya watu wote na inajali hivyo tunaimani kuwa changamoto zenu zitafikishwa mahali husika na zitajadiliwa na kupewa ufumbuzi ".Amesema
.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad