| Muhogo Mchungu kulia akiwa na msanii mwenzake habari maelezo Dar es Salaam |
MSANII mkongwe wa filamu nchini Tanzania Muhogo Mchungu
amesema kuwa yupo chimbo akijiaandaa kutoa kitabu kitakachowafundisha watanzania
wengi na kuwaburudisha wale wanaopenda
kusoma vitabu,
Msanii huyo amesema kuwa ana vipaji vingi na anatumia ili
kuwapa burudani wale wanaomkubali n amewataka wawe na subira kwa kuwa mambo
mazuri hayataki haraka baada ya muda kutimia kila
kitu kitakuwa sawa.
“Najiandaa kuandika kitabu changu ambacho kitakuwa ni
zawadi kwa watanzania ambao wanafuatilia na kupenda kazi zangu nipo kwa ajili ya
wananchi na watanzania watambue umuhimu wa kusoma vitabu ili kuongeza ujuzi
zaidi”.Amesema
Aidha amewasihi watanzania kuendelea kutazama na kufuatilia
filamu zake ambazo zipo sokoni na zinafanya vizuri sokoni ambapo ni pamoja na
ile After death
No comments:
Post a Comment