Mazoezi siri ya ushindi kwenye mpira - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Monday, 31 October 2016

Mazoezi siri ya ushindi kwenye mpira

                                               
Mwalimu wa Michezo Deus Malongo (Katikati) akiwafunda wachezaji wa DSJ stars katika viwanja vya Mlimani 

MWALIMU wa michezo wa chuo cha uandishi wa habari Dar es Salaam (DSJ)  Deus Malongo amewataka wanafunzi kuhakikisha wanafanya mazoezi na kujiweka sawa katika mazoezi ili waweze kujiweka sawa katika masuala ya michezo.

Akizungumza na wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari amesema kuwa michezo ni jambo la kuzingatia na kitu muhimu katika michezo ni mazoezi yanayomfanya mwanamichezo kuwa katika
hali nzuri ya kushiriki na kushinda.

“Mpira siku zote ni mazoezi ndiyo yanayofanya timu kuweza kushinda hivyo kuna umuhimu wa kufanya mazoezi ya mara kwa mara ili kujiimarisha na kuwa tayari kwa mashindano muda na wakati wowote “.Amesema.

Naye Ally Makame Naibu waziri wizara ya Michezo DSJ amesema kuwa wanatambua umuhimu wa mazoezi  hivyo wamejipanga kuwa na muda wa kufana mazoezi mara kwa mara ili kujiweka sawa kabisa .


“Tunatambua umuhimu wa mazoezi na tunathamini umuhimu wake hivyo mkakati wetu upo wazi na kila mchezaji anataarifa juu ya kufanya mazoezi na kushiriki mazoezi kujiweka sawa kwa ajili ya mechi na mashindano ya kirafiki”.Amesema

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad