VIJANA 50
walio nje ya shule wamefundishwa elimu ya uzazi na kujilinda na maambukizi ya
magonjwa ya zinaa pamoja na mimba za utotoni ili kuwafundisha wengine.
![]() |
| Mkurugenzi wa UNA Steve Mfuko |
Akizungumza
na mwandishi wa habari hii Mkurugezi wa UNA
(Uigizaji Ngoma Asilia) Steven Mfuko alisema kuwa wameamua kutoa mafunzo
kwa vijana ili kukuza ufahamu
wao kuhusu masuala ya afya.
wao kuhusu masuala ya afya.
“Tunatoa
mafunzo kwa vijana kuanzia miaka 12-23 kwa kuwafunza masomo ya afya ya uzazi
pamoja na mbinu za kujilinda dhidi ya magonjwa ya zinaa ambayo yamekuwa chanzo
cha kurudisha nyuma maendeleo”alisema
Alisema kuwa
wameamua kutoa elimu kwa vijana ili kuwapa ujuzi wa kutosha na kwa wale
watakaopata mafunzo wanajukumu la kuwafunza wengine ili ujuzi usipotee.
Rajabu Hamis
ambaye ni mwanafunzi katika mradi huo alisema kuwa wanafundishwa mbinu mbalimbali
kuhusiana na kirafiki zaidi juu afya ya uzazi hali inayowafanya waweze kuelewa
masomo yanayoendeshwa na asasi hiyo.
“Tunafundishwa
na walimu wenye uzoefu na waliobobea katika sekta ya afya hali inayotufanya
tuweze kuelewa masomo pamoja na kufurahia darasa”alisema Hamisi

No comments:
Post a Comment