AT awafunda wasanii - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Tuesday, 20 June 2017

AT awafunda wasanii



MSANII wa muziki wa mduara Ally Ramadhani anayetambulika kwa jina la AT amewataka wasanii kujitoa kwa ajili ya wenye uhitaji ili kuweza kupata thawabu kwa Mungu  kwa kuokoa maisha ya wanaoishi mazingira magumu.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi  alisema kila mmoja anapaswa kutambua kwamba  kujitoa kwa ajili ya wengine ni jambo la kheri  hakuna wa kuachiwa mzigo hasa linapokuja suala la kusaidia jamii.
Watoto wanaolelewa katika kituo cha Maunga Center kilichopo Kinondoni wakiwa katika michezo kukuza uwezo wa akili

“Kila mmoja anawajibu wa kutambua umuhimu wa kuwasaidia wale walio katika mazingira magumu  kukwepa majukumu na kuiachia serikali ama kikundi cha aina fulani hilo si jambo jema kwani wote tupo katika jamii”alisema AT.

Aidha alisema kuwa kujitoa hakuangalii umaarufu ama cheo cha mtu kila mtu ana wajibu  tabia za vizingizio kwa wasanii wakubwa zisipewe nafasi jambo linalotakiwa ni kuungana katika kila hali.


“Kwa mwenye kujali na kutambua umuhimu wa umaarufu wake anawajali wengine pia  tunapaswa kuunganisha nguvu zetu katika kuwasaidia wenzetu kwa kuwashika mkono na kuwafariji pia  hata muda nao ni zawadi tosha kwao”alisisitiza

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad