KATIBU wa Maunga Center ambacho ni kituo cha kulea watoto
yatima Rashid Mpinda amewataka wana
jamii kuwajali watoto walio katika
mazingira magumu kwani hilo ni agizo la Mungu kwa wote wenye dini na wasiokuwa
na dini.
| Michezo huimarisha afya ya watoto kama ambavyo walikutwa watoto wa kituo cha kulea yatima cha Maunga Center kilichopo Kinondoni wakicheza kiboleni |
Akizungumza na mwandishi wa habari hii alisema kuwa jukumu
la kuwatunza yatima ni letu sote na kwa kufanya hivyo tutakuwa tukitimiza
maagizo ambayo tuliachiwa na Mwenyezi Mungu hali
itakayotupa thawabu.
“Wajibu wa kuwatunza watoto ni wetu sote kuna ulazima wa kuungana pasipokubaguana kwa
kuwa sisi sote ni ndugu na wale walio katika mazingira magumu si kwa mapenzi
yao kwani hakuna anayependa kuishi maisha magumu”alisema Mpinda.
Aidha alisema kuwa serikali inapaswa kuvithamini vituo vya
watoto kwani uhitaji ni mkubwa siku zote wanakwama kuendelea kuwachukua watoto
wengine kutokana na uhaba wa eneo hali inayosababisha washindwe kutoa msaada.
“Uhitaji wa eneo kwa ajili ya makazi ya watoto unatufanya
tushindwe kuwasaidia watoto wengine hivyo tunapenda kuiomba serikali iweze
kutupatia eneo ambalo litatuwezesha kujenga kituo kikubwa zaidi na kutoa
matunzo kwa waliokosa nafasi”alisema Mpinda
No comments:
Post a Comment