Miss DSJ aitaka jamii kujiitoa kwa wahitaji - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Wednesday, 21 June 2017

Miss DSJ aitaka jamii kujiitoa kwa wahitaji


MLIMBWENDE wa chuo cha uandishi wa habari Dar es Salaam anayeshikilia taji la Miss DSJ 2016 – 2017 Anna Andrew amewataka wanajamii kuwa na utamaduni wa kuwatembelea wenye uhitaji .

Akizungumza na mwandishi wa habari hii alisema kuwa karibu nao kunawafanya waweze kutambua thamani yao kwa kujiona hawana tofauti  na  wengine ambao wanaishi kwenye mazingira bora.
Ana Andrew Miss DSJ

“Hakuna anayependa kuishi maisha ya upweke hivyo jamii yapaswa kutambua  kitendo cha kuwafikia wenye uhitaji kinaongeza furaha kwao pia ni kitendo kinachoonesha ukomavu wa upendo kwa ndugu zetu tunaoishi nao “alisema Anna

Stanley Ackson ambaye ni balozi wa Nishike Mkono alisema kuwa  imefika wakati wa kuonesha upendo kwa vitendo hasa kwa ndugu zetu ambao wanaishi katika mazingira hatarishi hali itakayoweza kuwainua wale waliokata tamaa.


“Maneno matupu hayawezi kutosha kwa kuwa kila mmoja ni bingwa wa kuongea kinachotakiwa ni utekelezaji na kuhakikisha kuwa matendo ndio yanapewa nafasi katika kila jambo kwani undugu kufaana kama ambavyo wahenga walisema “alisisitiza Ackson

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad