Ajira zinadumaza watoto - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Thursday, 22 June 2017

Ajira zinadumaza watoto

Dar es Salaam

KATIBU wa soko la Kisutu Suitbert  Nyawalle amewataka wazazi wenye tabia ya kuwaajiri watoto waache  kwani kwa kufanya hivyo kunamfanya awaze sana fedha hali inayodumaza uwezo wa kufikiria masomo .

Mtoto akiwa katika biashara ya Karanga
Akizungumza na mwandishi wa habari hii alisema kuwa mtoto mwenye umri chini ya 18 bado
anahitaji elimu na matunzo bora ili aweze kujijengea uwezo wa kufikiri pamoja na kutambua matumizi sahihi ya muda.

“Ukomavu wa akili katika suala la fedha unahitajika hasa kwa mtoto anatakiwa apewe muda mwingi kujifunza  sio kuwa katika ajira isiyo rasmi hivyo kuna umuhimu wa mzazi kutambua hilo na kumpa fursa ya kuendelea na masomo”alisema

Aidha alisema kuwa hakuna mfanyabiashara anayeruhusiwa kumwajiri mtoto katika soko hilo ikibainika anapewa adhabu kwani atakuwa anakiuka mipango ya uongozi pamoja na mkakati wa serikali katika kutokomeza ajira kwa watoto.


“Adhabu kali kwa anayekiuka agizo la uongozi inahusika kwani sheria ni msumeno inakata kote kote tuna jukumu la kuwalinda watoto na kuwapa elimu ili waweze kutusaidia baadaye na sio kuwafanya watutumikie kabla ya wakati”alisisitiza

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad