UWEZO wao mkubwa upo katika kufurahi na kusahau mabaya kwa
urahisi hali inayowafanya wajihisi wapo salama hata sehemu yenye hatari kubwa
ndio maana hata wakimwona mdudu kama nyoka wanacheka na kumfuata bila hofu.
| Uwezo wa kuunda magari ya kuchezea umefanywa na watoto hawa waliopo kituo cha kulea watoto Maunga Kinondoni |
Tupo nao kwenye jamii yetu kila siku kila saa wanahitaji
uangalizi mkubwa ili wazidi kuwa salama kwani tusipowajali hawa tunapoteza nasi
furaha kwa kutumia muda mwingi kuitafuta furaha ambayo
ilikuwa inachezewa nasi
wenyewe bila kujua.
Hakuna anayetambua thamani ya kile alichonacho mkononi ndio
maana wahenga kwa kulijua hilo
walisema “Mbuzi hakuona thamani ya mkia wake mpaka pale ulipoungua”ni fursa yetu kuwatunza hawa wadogo ambao ndio taifa la kesho.
walisema “Mbuzi hakuona thamani ya mkia wake mpaka pale ulipoungua”ni fursa yetu kuwatunza hawa wadogo ambao ndio taifa la kesho.
Mwimbaji makini na mwandika mashairi Judithi Mbibo wengi
wanamtambua kama Lady Jay dee aliandika mashairi akisema kuwa Mtoto ni malaika
hivyo kuna umuhimu wa kuwatazama kwa
umakini watoto kila wakati na si kipindi cha sikukuu tu.
“Nikichoka kutembea nabebwa,kulala muda niloamua ni vitu
ambavyo anavifanya mtoto kutokana na hali ya kupewa mamlaka ya kile
anachokitaka japo hana uwezo huo jukumu letu kubwa kuwatunza na kuhakikisha
wanatimiza ndoto zao”
No comments:
Post a Comment