LICHA ya jitihada kubwa ambazo zinafanywa na Jeshi la polisi
katika kuhakikisha kuwa ulinzi na usalama wa raia unaimirika hasa kipindi cha
sikukuu bado wananchi wamelitupia lawama jeshi hilo kwa kupuuzia usalama wa
watoto.
| Bado si salama maeneo ya kuogea watoto kwa kutokuepo kwa vifaa kama maboya ambayo endapo kutatokea na tatizo |
“Watotowengi wanapenda kucheza kwenye maji hivyo kuna umuhimu wa kuongeza usalama hasa
kwa kuweka maboya ambayo yatakua msaada kwa wazazi kuwasaidia watoto ama kuwepo
na jeshi la majini likifanya doria ”alisema Mohamed.
Ashura Ramadhani ambaye ni Mzazi alisema kuwa yupo karibu na
mwanaye ambaye anapenda kuogelea japo anacheza kwenye maji ya kina kifupi bado
anahofia endapo ataenda kwenye kina kirefu kwani yeye mwenyewe hajui kuogelea.
“Sina uwezo wa kuogelea mwanangu analilia kucheza kwenye
maji hali inayonilazimu nami pia niwe karibu naye hapa hivyo kuna haja ya maeneo
kama haya kuwekwa maboya ambayo yatakuwa msaada endapo litatokea tatizo”alisema
Ashura .
Kaimu kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lucas
Mkondya alisema kuwa Jeshi limejipanga vyema kuhakikisha wananchi
wanasherehekea sikukuu kwa amani bila
bugudha za ya aina yoyote.
“Uzoefu unaonesha kuwa mara nyingi kipindi cha sikukuu watu
wenye nia ovu hujiandaa kufanya vitendo vya kiarifu kutakuwa na doria ya masaa
24 maeneo yenye mikusanyiko mikubwa ya watu na tutatumia taarifa za
kiintelijinsia kuimarisha ulinzi”alisema Mkondya
No comments:
Post a Comment