MBUNIFU wa gazeti la Uhuru na mzalendo Kuruthum Matanda
amewataka wanafunzi wa chuo cha uandishi
wa habari Dar es Salaam (DSJ) kutumia ujuzi wao katika utendaji wa kazi ili
waweze kuwa tofauti na wengine katika tasnia ya uandishi wa habari.
![]() |
| Mbunifu kurasa Kuruthumu Matanda kushoto akiwaelekeza namna kazi inavyofanyika wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Dar es Salaam (DSJ) walipotembelea ofisi za Uhuru na Mzalendo |
Akizungumza na wanafnzi hao waliotembelea ofisi ya Uhuru katika ziara ya masomo alisema
kuwa kujifunza ni jambo lisilokuwa na kikomo kwa watu wote.
“Hakuna kitu kigumu hivyo ujuzi ambao unao ni mtaji tosha
katika kuhakikisha kuwa unafanikisha ndoto zako kwani hakuna kinachoshindikana
endapo utaamua kwa moyo wa dhati kufanya hi lo jambo”alisema
Athanas Kazige ambaye ni mhariri wa Michezo gazeti la Uhuru
na Mzalendo alisema kuwa wanafunzi wasizahau kanuni wanazofundishwa kuhusu
uandishi pamoja na kuongeza mbinu za kikomando katika kuhakikisha wanapata
ukweli.
“Mengi yanatokea hasa katika kutafuta habari jambo la
kuzingatia ni kuhakikisha unatumia mbinu kamili ambazo zitakupa nafasi ya
kupata kile unachohitaji ili uweze kuujuza umma kinachoendelea kwani kazi kubwa
ya mwandishi ni kuhakikisha anatoa taarifa za kweli”alisema Kazige.
Baraka Michel mwanafunzi wa ngazi ya cheti kwa chuo cha
uandishi wa habari Dar es Salaam alisema kuwa ziara za masomo zinawajenga
katika kuhakikisha kuwa wanatambua namna ya kutafuta habari mpaka kukamilika
kuripotiwa kwa jamii.

No comments:
Post a Comment