MHARIRI mkuu wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo Bakari Mkondo
amewataka wanafunzi kujituma kwa juhudi katika masomo na kazi ili waweze kufikia
malengo yao katika tasnia ya uandishi wa habari
![]() |
| Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Dar es Salaam wakifundishwa namna ya kubuni kurasa na msanifu wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo Kulthumu Matanda |
Akizungumza na wanafunzi wa chuo cha uadishi wa habari Dar
es Salaam (DSJ) waliofanya ziara ya
masomo ofisini hapo alisema kuwa fani ya uandishi inamtaka mwanafunzi kujitoa
na kuhakikisha
thisisdizo444@gmail,comkuwa anatumia muda mwingi kufikiria kufanya vizuri .
“Kujifunza ni siku zote hivyo kuna haja ya kuhakikisha kuwa
mazoezi yanafanywa kwa vitendo hasa kwa kuandika habari ambazo zinafuata misingi ya uandishi wa
habari ambazo zinazingatia kanuni hazina
dalili ya udanganyifu katika tasnia ya uandishi”alisema Mkondo.
Mhariri wa habari Stephen Baligeya aliwataka wanafunzi
kuzingatia miiko ya uandishi wa habari ili kuweza kuepuka kesi zisizo za lazima
katika uandishi jambo ambalo sio jema kwa mwandishi aliyekaa darasani.
“Umakini wa kuzingatia maadili hasa katika uandishi ni kitu
cha msingi kwani hakuna kazi isiyozingatia maadili haiwezi kupata nafasi ya
kumtambulisha mwandishi katika tasnia zaidi ya kushusha hadhi yake ya
taaluma”alisema
Ana Andrew ambaye ni balozi wa chuo cha uandishi wa habari
Dar es Salaam alisema kuwa ziara imemuongezea ujuzi hasa kwa kuweza kujifunza
namna ya mpangilio wa gazeti unavyokuwa na mbinu za uandishi wa habari ambazo
zitakuwamwongozo katik kazi yake.

No comments:
Post a Comment