Mwakifamba atema cheche kwa wasanii - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Monday, 3 July 2017

Mwakifamba atema cheche kwa wasanii


RAIS wa shirikisho la filamu Tanzania(TAFF) Simon Mwakifamba amewataka wasanii  kuokwenye kazingeza juhudi  kwa kuongeza ujuzi wa kutengeneza filamu pamoja na kubadilisha aina za wahusika wakuu wanaowatumia kuchezaza filamu.

Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Simon Mwakifamba
Akizungumza na wasanii wa filamu  na wadau wa sanaa katika ukumbi wa Baraza la Sanaaa Taifa  alisema mapito wanayopitia wasanii yatakwisha  ni ya muda kutokana na kile ambacho kimepandwa na wasanii wenyewe hali inayofanya wavune maumivu kwa kushindwa kutengeneza kazi zenye utofauti.

“Watazamaji wamekuwa na ujuzi mkubwa kuliko watengeneza filamu hali inayosababisha kazi kudorora sokoni hivyo ili kuweza kulishinda jambo hili kuna ulazima wa kuwa wabunifu kwa kujifunza bila kuchoka ili waweze kutengeneza kitu cha kipekee”alisema Mwakifamba.

Alisema kuwa kukua kwa sanaa kunategemea na dhamira ya msanii mwenyewe kwa kile anachokiamini ndiko kunaweza kuleta mabadiliko  sio kuishia kulalamika kuwa hakuna mauzo ilihali wasanii wenyewe ni wachangiaji .

“Ili kufikia mabadiliko lazima tujiandae kwenye fikra sio kuwa na mawazo finyu ambayo sio chachu ya kuelekea kule tunakohitaji lazima tukubali kuwa tumekosea tujipange upya kuboresha yale ambayo ni mapungufu yetu”alisema


Alisema kuwa kutokubali kuibua vipaji vipya kunaiponza tasnia ya filamu kwani waigizaji wenye majina wamekuwa wakirudia kucheza filamu hali inayofanya kushindwa  kutofautisha aina ya filamu kwa kuwa hakuna kitu cha kuwatofautisha katika kazi mpya.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad