NAIBU katibu mkuu wa wizara ya maliasili na utalii Aloyce
Nzuki amesema kuwa Serikali ina mpango wa kuinua kipato cha nchi kupitia
sekta ya utalii ambayo ina fursa nyingi zinazoweza kuinua uchumi wa nchi kwa
kiasi kikubwa.
Akizungumza Da r es salaam katika ukumbi wa mikutano wa
shirika la kazi Duniani(ILO) kwenye uzinduzi wa ripoti ya maendeleo ya kiuchumi ya UNCTAD 2017 ambayo imeangazia sekta ya utalii na
uchumi alisema kuwa utalii ni miongoni mwa raslimali ambayo inauwezo wa
kuongeza
mapato kupitia kodi.
“Tuna sehemu nyingi
zenye vivutio hali ambayo inaweza kuongeza mapato kwani sehemu kubwa inayotumika kwa sasa kufanyia utalii kuwa ni kanda za kaskazini
pekee hivyo tuna mradi wa kuongeza sehemu za kanda ya Magharibi pamoja na Kusini”.
Alisema kuwa wamegundua sehemu nyingine ambayo ni kivutio
zaidi kwa watalii kama fukwe za bahari ambazo zipo kandokando ya bahari ya
hindi maeneo ya Dar es Salaam pamoja na Tanga ambayo hayatumiki katika shughuli
za utalii hivyo wapo kwenye mkakati kuyachukua.
Prosper Charle ambaye ni mchumi katika masuala ya maendeleo
alisema kuwa Tanzania ipo kwenye kufanya mageuzi ya uchumi katika sekta ya
viwanda hivyo kuna haja ya kupanua wigo wa mapato ambapo utalii pia ni miongoni
mwa sekta inayoweza kuleta maendeleo.
“Endapo kutakuwa na maboresho hasa kwenye miundombinu itakuwa ni kivutio kikubwa kwa watalii kuweza
kufika maeneo bila wasiwasi hali
itakayoongeza idadi ya watalii kuweza kufika kwenye maeneo yenye vivutio
pamoja na kuwekeza kwenye utalii wa ndani”alisema

No comments:
Post a Comment