YANGA YAINYOOSHA MLANDEGE ZANZIBAR - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Wednesday, 10 November 2021

YANGA YAINYOOSHA MLANDEGE ZANZIBAR

 


HERITIER Makambo nyota wa Yanga alipachika bao pekee la ushindi katika mchezo wa kirafiki uliochezwa Uwanja Aman dhidi ya Mlandege FC ya Zanzibar. 


Katika mchezo huo dakika 45 za awali ngoma ilikuwa ngumu kwa pande zote mbili kupenya katika nyavu na kuwafanya waende mapumziko wakiwa wametoshana nguvu.


Ilibidi Yanga wasubiri mpaka dakika ya 49 kupata bao la ushindi kupitia kwa Makambo ambaye alipachika bao hilo akiwa ndani ya 18 na likajaa nyavuni.


Shuti la Fiston Mayele akiwa ndani ya 18 liligonga mwamba na kurudi ndani ya uwanja mpira huo ukakutana na Makambo ambaye alimshukuru Mayele kwa mpira wake aliopiga kwa mguu wa kulia kugonga mwamba yeye akamalizia kwa mguu wa kushoto.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad