UWANJA wa Kaitaba dakika 90 zimekamilika mbinu ya Pablo Franco imekwama mbele ya Kagera Sugar.
Ni Hamis Kiiza dakika ya 70 aliwatungua Simba baada ya safu ya ulinzi kufanya makosa katika kuokoa shambulizi la kushtukiza.
Hakuna sababu nyingine kwa Franco ambaye alikuwa kwenye uwanja mzuri wa kapeti wa Kaitaba kakwama kushinda ugenini.
Simba inabaki na pointi zake 25 ikiwa imecheza mechi 13 na vinara ni Yanga wenye pointi 35.
Kiiza alionyeshwa kadi nyekundu baada ya kuonyeshwa kadi mbili za njano.
No comments:
Post a Comment