BAADA ya ushindi ambao wameupata mbele ya Tanzania Prisons kikosi hicho kimeibukia Mtwara.
Yanga ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons mtupiaji akiwa ni Feisal Salum dakika ya 89 na kuipa ushindi timu hiyo.
Sasa Yanga ni vinara wa ligi wakiwa wamecheza mechi 14 n kibindoni wana pointi 35 wanakutana na Namungo ambayo imekusanya pointi 15 zote zikiwa zimecheza mechi 14.
Namungo imetoka kunyooshwa mabao 3-0 dhidi ya Singida Big Stars kwenye mchezo wao uliopita uliochezwa Uwanja wa Liti.
Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Desemba 7, Uwanja wa Majaliwa.

No comments:
Post a Comment