YANGA NDANI YA MTWARA - Dizo Click

Dizo Click

Hot

Post Top Ad

Monday, 5 December 2022

YANGA NDANI YA MTWARA

 


BAADA ya ushindi ambao wameupata mbele ya Tanzania Prisons kikosi hicho kimeibukia Mtwara.


Yanga ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons mtupiaji akiwa ni Feisal Salum dakika ya 89 na kuipa ushindi timu hiyo.


Sasa Yanga ni vinara wa ligi wakiwa wamecheza mechi 14 n kibindoni wana pointi 35 wanakutana na Namungo ambayo imekusanya pointi 15 zote zikiwa zimecheza mechi 14.


Namungo imetoka kunyooshwa mabao 3-0 dhidi ya Singida Big Stars kwenye mchezo wao uliopita uliochezwa Uwanja wa Liti.


Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Desemba 7, Uwanja wa Majaliwa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad