KATIKA anga la kimataifa wakiwa na pointi tano kundi D wawakilishi wa Tanzania kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika Yanga wameweka wazi kuwa malengo yao ni kutinga hatua ya robo fainali Ligi ya Mabingwa Afrika.
Mchezo ujao kwa Yanga katika anga la kimataifa ikiwa
hatua ya makundi ni dhidi ya CR Belouzidad unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa
Mkapa.
Timu zote mbili zina pointi tano kibindoni hivyo
mshindi ataongeza nafasi ya kufikia malengo ya kutinga hata ya robo fainali.
Ali Kamwe Ofisa Habari wa Yanga amesema:" Kundi
la kiume ambalo tupo na nafasi bado iko wazi kwa kila timu. Sisi Yanga
fainali yetu ni Uwanja wa Mkapa Vs Belouzidad.
"Mchezo huo utakuwa ni 24/2/2024. Mpango wetu
ni robo fainali. Na tutautimiza mpango huu kama tutaungana pamoja na kwenda
Uwanjani kuwapa nguvu wachezaji wetu siku hiyo.
"Uwanja kujaa ndio silaha yetu ya kwanza ya kumpunguza makali Mwarabu,
mashabiki tujitokeze kwa wingi muda ni sasa,".
No comments:
Post a Comment